Singida Black Stars, KMC vita mpya Ligi Kuu Bara

UTAMU wa Ligi Kuu Bara unaendelea tena leo kwa michezo miwili, huku macho ya mashabiki yakiwa kwenye Uwanja wa Liti mjini Singida wakati Singida Black Stars itakapovaana na KMC, huku kocha Patrick Aussems akitamba kuendeleza ubabe. KMC mazoezini Singida ilianza msimu kwa kishindo kwa kupata ushindi katika mechi mbili mfululizo ikiwa ugenini, ikianza kwa kuichapa…

Read More

Makambo aanza kuiona tofauti ubora Ligi Kuu Bara

MSHAMBULIAJI wa Tabora United, Heritier Makambo ‘Mzee wa Kuwajaza’ amesema kuna mabadiliko makubwa ya ubora katika Ligi Kuu Bara kulinganisha na misimu kadhaa nyuma alipokuwa na kikosi cha Yanga.Makambo ameitumikia Yanga kwa misimu miwili tofauti baada ya kuuzwa Horoya ya Guinea na baadaye akarejea tena nchini na kuondoka kwenda Uarabuni kabla ya hivi karaibuni kurudi…

Read More

Hii Taifa Stars usiikatie tamaa

GHAFLA Taifa Stars imepindua meza kibabe na kurudi njia kuu kwenye matumaini ya kufuzu ushiriki wa Fainali za Mataifa Afrika, baada ya kuichapa Guinea kwa mabao 2-1 tena ikiwa ugenini. Mchezo huo wa Kundi H ulipigwa huko Ivory Coast, kulikochaguliwa na Guinea kuwa uwanja wa nyumbani, huku ikitoka kupoteza mbele ya DR Congo wakati Tanzania…

Read More

Changamoto ya malazi Singida yaikwamisha KMC Dodoma

Kikosi cha KMC kimeendelea kusalia Dodoma baada ya kukosa sehemu ya malazi mjini Singida ambako itacheza kesho dhidi ya Singida Black Stars mchezo wa Ligi Kuu Bara. Kwa mujibu wa ofisa habari wa timu hiyo, Khaleed Chukuchuku, wameshindwa kusafiri leo kwenda Singida kwakuwa timu imekosa mahali pa kufikia. “Tumeshindwa kufika kituo cha mechi mpaka muda…

Read More

Madina ala kiapo Tanzana Open

MASHINDANO ya gofu ya wazi kwa wanawake yanaanza kesho katika viwanja vya gofu vya Arusha Gymkhana, huku Tanzania ikiwa na mtihani wa kuthibitisha ubora nyumbani baada ya kufanya vizuri viwanja vya ugenini. Madina Iddi ambaye ni bingwa wa mataji matatu  Zambia na Uganda, amesema wako imara kwa mashindano hayo ambayo pia yataiwezesha Tanzania  kupata kikosi…

Read More

Wababe wa magari waanza kutua Iringa

HOMA ya mbio za magari Iringa inazidi kupanda wakati madereva na wasoma ramani wakianza kuwasili leo kabla ya vita ya injini mwishoni mwa wiki. Kuongezeka kwa dereva mkongwe Himid Mbatta wa Iringa na wakali Altaf Munge, Shehazad Munge  na Manveer Birdi kutoka Dar es Salaam kunaweza kumpa wakati mgumu bingwa mtetezi Yassin Nasser ambaye awali…

Read More

Mikumi safi majaribio timu ya taifa kriketi

TIMU ya Mikumi imepata ushindi wa tatu dhidi ya Ngorongoro katika kriketi, ambapo safari hii imeshinda kwa wiketi mbili kwenye Uwanja wa Dar Gymkhana. Timu hizo za kombani zinaundwa na wachezaji nyota wa kriketi nchini kama maandalizi ya timu ya taifa kwa michuano ya kufuzu Kombe la Dunia zitakazochezwa Dar es Salaam mwishoni mwa mwezi…

Read More

Robo ya nne yaikosesha ushindi UDSM

UZEMBE wa wachezaji wa UDSM Outsiders kwa kufanya madhambi katika robo ya nne ulichangia timu hiyo kupoteza mchezo dhidi ya Savio kwa pointi 69-65. Mchezo huo wa Ligi ya Kikapu Dar es Salaam, uliofanyika katika Uwanja wa Donbosco, Upanga, wachezaji Mwalimu Heri na Tryone Edward walifanya madhambi mara nne, jambo lililowafanya wacheze kwa woga wakihofia…

Read More

Timu tano zatangulia nane bora BDL

WAKATI zimebaki mechi tatu ili kumalizika kwa michezo 30 ya Ligi ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BDL) kwa kila timu, tayari klabu tano zimetinga hatua ya nane bora. Timu hizo ni Dar City yenye pointi 51, UDSM Outsiders (51), Savio (49), Mchenga Star (50) na JKT (46). Nafasi za timu hizo zimepatikana baada…

Read More

Mchenga yatamba kuwanyoosha wapinzani BDL

BAADA ya Mchenga Star kupata ushindi wa pointi 84-64 dhidi ya Ukonga Kings katika mchezo wa Ligi ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BDL), kocha mkuu wa timu hiyo, Mohamed Yusuph amesema kwa sasa nguvu wamezielekeza katika   michezo mitatu iliyobaki akiahidi ushindi. Akizungumza na Mwanasposti katika Uwanja wa Donbosco Oysterbay, alisema mkakati wao kuhakikisha…

Read More