Maswali yalivyowavuruga wagombea Chadema | Mwananchi

Dar es Salaam. Usaili wa wagombea wa uenyekiti, umakamu na wahazini wa kanda nne za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ngoma nzito ndivyo unavyoweza kusema. Hii inatokana na mchakato kuchukua muda mrefu tofauti na matarajio ya wagombea na hofu ya watia nia kupenya. Usaili huo hauna tofauti na uliofanyika jana Jumapili, Mei 12, 2024…

Read More

ZIMAMOTO WAZINDUA NYUMBA ZA MAKAAZI NA MAGARI.

DODOMA. Mei 13, 2024 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe.Mhandisi Hamad Masauni (Mb) amezindua Nyumba za Makaazi ya Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji zilizopo Kikombo Jijini Dodoma. Uzinduzi huo umefanyika sambamba na uzinduzi wa Magari 12 ya kuzimamoto, yakiwemo Magari mawili ya Ngazi yenye uwezo wa kufanya maokozi katika Majengo Marefu…

Read More

Israel yaendelea kushambulia Rafah – DW – 13.05.2024

Asubuhi ya Jumatatu , anga la Gaza lilikuwa limetanda moshi kutokana na mashambulizi ya mabomu na mizinga yaliyofanywa na jeshi la Israel, wakati likijaribu kujipenyeza ndani ya mji wa kusini wa Rafah kwa kile msemaji wake, Daniel Hagari, alichokiita kuwa ni “operesheni maaluum”, na kuwafanya wakimbizi wa ndani wa Kipalestina kukimbia huku na kule kutoka kwenye…

Read More

Madaktari bingwa 35 kutoa matibabu bure Mbeya

Mbeya.  Timu ya madaktari bingwa  35 imewea  kambi ya siku tano jijini hapa kwa ajili   ya kutoa huduma  bure za  uchunguzi na matibabu ya  kibingwa kwa wananchi. Kambi hiyo imeanza leo Jumatatu Mei 13, 2024 itadumu hadi Mei 17 mwaka huu  na itahusisha  hospitali zote za wilaya zilizopo katika halmashauri saba za Mkoa wa Mbeya….

Read More

DC KASILDA AKERWA NA RUWASA SAME KUTOSHIRIKISHA JAMII KATIKA MIRADI YAKE.

NA WILLIUM PAUL, SAME. MKUU wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro Kasilda Mgeni ameeleza kusikitishwa na kitendo cha Wakala wa maji safi na usafi wa Mazingira vijijini (RUWASA) wilayani humo kushindwa kushirikisha jamii husika kwenye maeneo mbalimbali ambako kunatekelezwa miradi ya maji hali inayopelekea kutokea malalamiko kutokana na kutoelewa nini kinaendelea. Kasilda ameeleza hayo baada…

Read More

Zelensky asema jeshi lake liko katika vita ‘vikali’ mpakani – DW – 13.05.2024

Vita hivyo vikali vinatokana na mashambulizi ya vikosi vya Urusi vinavyojaribu kusonga mbele katika vijiji vya mpaka wa jimbo la Kharkiv.  Mashambulizi mapya ya Urusi Kaskazini mashariki mwa jimbo la Kharkiv, pamoja na msukumo wake unaoendelea katika mkoa wa mashariki Donetsk, vinajiri baada ya miezi kadhaa, kabla ya kutopiga hatua yoyote kwenye uwanja wa mapambano wa…

Read More

Bei ya ufuta yafurahisha wakulima

Mtwara. Baada ya ufuta kuuzwa kwa Sh4,000 katika mikoa ya Lindi na Mtwara msimu uliopita Mkoa wa Songwe umeweka rekodi kwa kuuza zao hilo kwa Sh4,500 kwa kilo msimu huu hali ambayo inaongeza matumaini kwa wakulima.  Akizungumza na Mwananchi  Digital, Mratibu wa programu ya ufuta kitaifa kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (Tari) Kituo…

Read More

Gamondi anusurika, waamuzi wafungiwa | Mwanaspoti

Kocha wa Yanga, Miguel Gamondi amepishana na adhabu ya kifungo baada ya kupigwa faini ya Sh2 milioni kwa kosa la kufanya vurugu ikiwemo kuwashambulia kwa maneno makali waamuzi wa mchezo dhidi ya Kagera Sugar adhabu iliyotolewa na Kamati ya Uendeshwaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi. Adhabu hiyo itashusha presha kwa viongozi na…

Read More