Serikali ilivyojipanga uboreshaji milki za ardhi

Dodoma. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imesaini mkataba wa Sh346 bilioni na Benki ya Dunia (WB) kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi. Mradi huo unalenga kuimarisha usalama wa milki za ardhi na kuwezesha miundombinu ya usimamizi wa rasilimali hiyo nchini. Majaliwa amesema hayo leo Juni 28, 2024…

Read More

Jeshi la Polisi lapiga marufuku kumiliki gobore, laruhusu Shortgun

Dar es Salaam. Jeshi la Polisi limepiga marufuku kampuni binafsi za ulinzi zinazotumia silaha zilizotengenezwa kienyeji (Gobore), badala yake imeshauriwa kufuata utaratibu wa kisheria wa kumiliki silaha aina ya “shotgun” kwani ndizo zinazoruhusiwa kutumika kwa shughuli za ulinzi. Pia, Jeshi la Polisi linawakumbusha wananchi kusalimisha silaha zilizokuwa zinamilikiwa kihalali na ndugu zao ambao kwa sasa…

Read More

Wananchi Mbeya wahaha kusaka maji usiku

Mbeya. Wananchi wa mitaa ya Mponzi, Sinde, Chaula na Makunguru jijini Mbeya wameendelea kusotea huduma ya maji kwa zaidi ya miezi miwili tangu kukatika kwake, huku wanawake wakielelezea hofu yao kiusalama wanapoamka usiku kutafuta huduma hiyo. Huduma hiyo ambayo ilipotea tangu Machi 2024 kwa baadhi ya maeneo, haijarejea tena na kufanya wakazi wa maeneo hayo…

Read More

Serikali, mabalozi kukutana kujadili changamoto za uwekezaji

Dar es Salaam. Wakati mabalozi wanaowakilisha mataifa yao Tanzania wameomba kukutana na Serikali kujadili changamoto zinazowakabili wawekezaji wa kigeni, Serikali imesema imelichukua suala hilo kwa umuhimu wa kipekee. Katika barua ya Juni 26, 2024, kwenda kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba, mabalozi hao wamesema licha ya ongezeko la…

Read More

Pingamizi mgombea ADC lapuuzwa, wanachama 197 kuamua

Dar es Salaam. Wakati wapiga kura 197 wakitarajia kufanya uamuzi wa kikatiba kumchagua mwenyekiti mpya wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Kamati ya uchaguzi huo imesema pingamizi alilowekewa mmoja wa wagombea wa nafasi ya mwenyekiti, Shabani Haji Itutu halijafuata kanuni za chama. Itutu aliwekewa pingamizi na wanachama saba wa ADC, Ibrahim Pogora, Asha…

Read More

Serikali yakiri upungufu wa maprofesa, yaanika mikakati kuukabili

Dar es Salaam. Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Nombo amekiri kwamba kuna uhaba wa wahadhiri nchini, hata hivyo amesema Serikali imechukua jitihada za kuhakikisha wataalamu kutoka nje wanakuja nchini kutoa mafunzo. Japo hakutoa takwimu ya upungufu uliopo wa wahadhiri nchini, Profesa Nombo amesema hatua nyingine ambayo Serikali imechukua ili uhaba…

Read More

BUNGE LAIDHINISHA MUSWADA WA SHERIA YA FEDHA WA MWAKA 2024

Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akisoma Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2024, ambao umepitishwa na Bunge baada ya kujadiliwa mara ya pili, bungeni jijini Dodoma. Muswada huo unatarajiwa kufanya marekebisho ya sheria za kodi ili kuwezesha utekelezaji wa kisheria wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2024/2025. Waziri wa Fedha…

Read More

Kaya 394,000 kuchomolewa orodha ya Tasaf

Iringa. Baada ya tathmini kuonyesha kaya 394,000 zimeweza kujimudu kiuchumi, Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) unatarajia kuziondoa katika mpango huo. Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tasaf, Shadrack Mziray amesema Juni, 2024 utakuwa wa mwisho kwa kaya hizo kupokea fedha kutoka Tasaf, hivyo kuanza kujitegemea. Akizungumza leo Juni 28, 2024 wakati wa ziara ya wadau wa…

Read More

Biashara Tunduma zarejea maduka yafunguliwa

Wafanyabiashara wa mkoa wa Songwe katika masoko yaliyopo Tunduma wilayani Momba wameungana na wenzao wa mikoa mingine ikiwemo Kariakoo kufungua maduka baada ya serikari kuahidi kufanyia kazi changamoto zao.  Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe … (endelea). Hatua hiyo imekuja ikiwa zimepita siku tatu za mgomo wa wafanyabiashara hao kuanzia tarehe 24 hadi 27n  Juni mwaka huu,…

Read More

Washtakiwa mauaji ya Milembe wajitetea, waomba kuachiwa huru

Geita. Washtakiwa wanne wanaodaiwa kumuua Milembe Suleman (43) kwa kumkata na kitu chenye ncha kali, wamejitetea wakieleza kutohusika na tukio hilo, wakiiomba mahakama iwaachie huru. Wamewasilisha ombi hilo mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Geita, Kelvin Mhina walipotoa utetezi wenyewe mahakamani hapo. Juzi, upande wa mashtaka ulifunga ushahidi ukiwa na mashahidi 29…

Read More