Jinsi baiskeli ilivyomsaidia kupambana na fisi kwa saa tatu

Sengerema. Bahati Kanfumu, mkazi wa Kijiji cha Kabusuli, Kata ya Nyamatongo, wilayani Sengerema, Mkoa wa Mwanza ameeleza jinsi alivyonusurika kushambuliwa na kundi la fisi. Akizungumza jana Agosti 11, 2024, amesema wakati akielekea kutafuta mahitaji ya familia asubuhi, alikutana na kundi hilo la fisi linalosadikika kuwaua watu wawili. Amesema alilazimika kushuka kutoka kwenye baiskeli aliyokuwa akiendesha…

Read More

Hatima dhamana ya kada wa Chadema aliyedaiwa kutekwa Agosti 22

Dar es Salaam. Hatima ya dhamana ya mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoani Tanga, aliyeripotiwa kupotea kabla ya Jeshi la Polisi Tanga, kutangaza kumshikilia siku 29 baadaye, na kisha kumfungulia kesi ya jinai, Kombo Mbwana sasa itajulikana Alhamisi Agosti 22,2024. Mahakama ya Wilaya Tanga siku hiyo itatoa uamuzi wa pingamizi la dhamana…

Read More

DPP amfutia mmoja kesi ya kusafirisha kilo 58.62 za heroini

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imemfutia kesi na kumwachia huru, Paulina Mwanga (38), aliyekuwa akikabiliwa na shtaka la kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroini zenye uzito wa kilo 58.62 Mshtakiwa huyo amefutiwa kesi hiyo, leo Jumatatu Agosti 12, 2024, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DDP), kuieleza Mahakama hiyo kuwa…

Read More

Wachimbaji Misungwi wagomea fidia ya Sh2 milioni

Mwanza.  Wachimbaji wadogo 32 wanaodai kumiliki eneo la machimbo ya dhahabu ya Shilalo wilayani Misungwi, wamegoma kupokea fidia ya Sh2 milioni kumpisha mwekezaji kutoka kampuni ya ChinaTanjikuangye. Wakizungumza kwa nyakati tofauti wachimbaji hao wamesema fidia hiyo ni ndogo na wanaomba Serikali iweke wazi mkataba ili wajue asilimia watakayoipata kwenye uwekezaji huo. Mgodi huo uliopo Kijiji…

Read More

Dk Nchimbi amwagiza Waziri Masauni awaachie viongozi Chadema

Geita. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi amemwagiza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Daniel Sillo kuzungumza na waziri wake, Hamad Masauni, ili kuona namna ya kuwaachia viongozi wa Chadema waliokamatwa mkoani Mbeya, akiwamo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe. Dk Nchimbi ameeleza hayo leo Jumatatu Agosti 12, 2024 alipozungumza kwenye…

Read More