Wenye ulemavu Mirerani walia mwenzao kudaiwa kuchinjwa na mwenza wake
Mirerani. Walemavu wa mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wamelalamikia kitendo cha mlemavu mwenzao Fatuma Saidi (28) kuuawa kwa kuchinjwa shingoni na mwanaume aliyekuwa anaishi naye. Mwenyekiti wa walemavu wilayani Simanjiro, Robert Matheus akizungumza na Mwananchi digital amesema anasikitishwa kwa tukio hilo la mauaji lililotokea leo Ijumaa saa moja asubuhi, Agosti 9, 2024…