Ngoma ya Magoma na Yanga ilikuwa hivi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeruhusu Klabu ya Yanga kufanya mapitio ya marejeo ya shauri la madai namba 187/2022 lililofunguliwa na Juma Magoma na mwenzake Geofrey Mwaipopo. Pia mahakama hiyo imetupilia mbali mwenendo mzima wa kesi hiyo ya madai namba 187/2022 na kuweka kando amri zote zilizotolewa katika katika hukumu iliyotolewa Agosti 2, 2023. Kuhusu…

Read More

Madai ya wananchi 328, KIA bado ngoma nzito

Moshi. Mahakama Kuu imewaidhinisha wananchi 10 kuwawakilisha wenzao 318 katika shauri la madai dhidi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) na Kampuni ya Uendeshaji Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KADCO). Kwa zaidi ya miaka 20 sasa, kumekuwapo mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wanaoishi vijiji vinavyozunguka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa…

Read More

Afariki dunia kwa kutumbukia kwenye kisima cha mafuta

Moshi. Mtu mmoja anayejulikana kwa jina la Shalom Tarimo (21), mkazi wa Msaranga, Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro amefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye kisima, kilichokuwa kikitumika kuhifadhia mafuta katika kituo kimoja cha mafuta kilichopo katikati ya mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro. Kisima hicho katika kituo hicho kinachodaiwa kumilikiwa na mfanyabiashara mmoja maarufu wa Moshi,…

Read More

NYUMA YA PAZIA: Pepe, kizazi cha mwisho cha masela wa ghetto?

MACHOZI yake baada ya mechi iliyowatupa Ureno nje michuano ya Euro pale Ujerumani yalikuwa machozi ya mwisho katika soka. Hatujua. Labda alilia zaidi kwa sababu alijua ilikuwa mechi yake ya mwisho katika soka. Pepe. Mreno kichaa. Mreno jeuri. Aliwahi kuandika Ben Mtobwa. ‘Machozi ndio njia pekee imalizayo huzuni ya mwanamke’. Hapana. Alikosea. Hata wanaume wanatoa….

Read More

Nyundo tano za Rais Samia Sikukuu ya Wakulima Nanenane

Na Nora Damian, Mtanzania Digital Dodoma Rais Samia Suluhu Hassan amehitimisha Sikukuu ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi (Nanenane) kwa mwaka 2024 akisema serikali imepiga hatua kubwa ambazo zimeanza kuleta matokeo mazuri huku dhamira yake ikiwa ni kujenga uchumi jumuishi katika sekta hizo muhimu. Akihutubia Agosti 8,2024 wakati wa kilele cha sikukuu hiyo kwenye viwanja vya…

Read More

Teknolojia yatajwa kupaisha kilimo, ufugaji

Unguja. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla amesema teknolojia imeleta mabadiliko katika sekta ya kilimo na ufugaji. Hemed amesema hayo baada ya kutembelea na kukagua bidhaa za kilimo na ufugaji leo Agosti 9, 2024 katika maonyesho ya wakulima Nanenane katika viwanja vya Dole Kizimbani, Unguja. Amesema maonyesho hayo yanatoa fursa kwa…

Read More