Hiki hapa kinaweza kuing’oa CCM Ikulu 2025
Miongoni mwa wabunge waliopata umaarufu katika Bunge la mwaka 2015 – 2020, ni Selemani Bungala, maarufu kama Bwege, aliyekuwa mbunge wa Kilwa Kusini kupitia Chama cha Wananchi (CUF) kabla ya kutangaza kuhamia ACT Wazalendo baada ya Bunge kuvunjwa. Bwege alijipatia umaarufu kupitia mtindo wake wa kuchangia hoja bungeni uliokuwa ukiwachekesha wabunge na watu wengine wanaomsikiliza…