
TARURA YAKAMILISHA UJENZI WA DARAJA LA MSADYA, MKOMBOZI KWA WANANCHI WA MPIMBWE
Mpimbwe, Katavi Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imekamilisha ujenzi wa daraja la Msadya lenye urefu wa mita 60 na upana mita 10.5 pamoja na ujenzi wa barabara unganishi ya Kibaoni-Chamalendi-Mdede kwa gharama ya shilingi bilioni 4.2 katika Halmashauri ya Mpimbwe mkoani Katavi. Meneja wa TARURA Wilaya ya Mlele, Mhandisi Paul…