Mapya mauaji ya mfamasia, mama afichua

Dar es Salaam. Kutokana na utata unaozunguka kifo cha aliyekuwa mfamasia wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke (TRRH), Magdalena Kaduma, mama yake mzazi ameelezea jinsi alivyopokea taarifa za kupotea kwa binti yake. Magdalena alitoweka Desemba 3, 2024, nyumbani kwake Kibamba, jijini Dar es Salaam, mwili wake ulipatikana ukiwa umefukiwa pembezoni mwa nyumba aliyokuwa…

Read More

Mwigulu aongoza  kumuaga ofisa TRA

Dar es Salaam. Mwili wa aliyekuwa mtumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Aman Simbayao aliyefariki dunia kwa kushambuliwa na wananchi wenye hasira eneo la Tegeta kwa Ndevu, jijini Dar es Salaam, umeagwa leo Jumapili Desemba 8, 2024 jijini Dar es Salaam. Shughuli ya kuaga mwili huo imefanyika viwanja vya michezo vya TRA Kurasini kuanzia…

Read More

DKT. NCHEMBA ASHIRIKI KUMUAGA MTUMISHI WA TRA

Waziri wa fedha Dkt. Mwigulu Nchemba akiwafariji wafiwa mara baada ya kuaga mwili wa  aliyekuwa mtumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Aman Kamguna Simbayao leo Desemba 08, 2024 katika Viwanja vya Michezo TRA vilivyopo Kurasini jijini Dar es Salaam. Amani alifariki Dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Mifupa -Moi-Dar es salaam baada kushambuliwa…

Read More

Familia mtumishi wa TRA yasema inamwachia Mungu

Dar es Salaam. Familia ya aliyekuwa mtumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Aman Simbayao imesema inamuachia Mungu kwa kile kilichotokea kwa ndugu yao, huku Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akitaka inunuliwe bondi ya Sh200 milioni kusomesha watoto. Simbayao alifariki Desemba 5, 2024 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam (MNH) alipokuwa…

Read More

Dakika 5 tu, zaitibulia Simba Algeria

MABAO mawili yaliyofungwa ndani ya dakika tano za kipindi cha pili, yaliitibulia Simba kutoka na ushindi ugenini baada ya kufungwa 2-1 na CS Constantine katika mechi ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika iliyopigwa kwenye Uwanja wa Mohamed Hamlaoui uliopo mji wa Constantine, Algeria. Kipigo hicho kimekuwa ni muendelezo mbaya kwa timu za…

Read More