
PATA HABARI MOTO MOTO KATIKA MAGAZETI YA LEO DISEMBA 27,2024
Home » PATA HABARI MOTO MOTO KATIKA MAGAZETI YA LEO DISEMBA 27,2024 About the author
Home » PATA HABARI MOTO MOTO KATIKA MAGAZETI YA LEO DISEMBA 27,2024 About the author
Rombo. Miili sita kati ya tisa ya watu waliofariki kwa ajali ya gari iliyohusisha basi la abiria la Ngasere na Toyota Noah, katika eneo la Tarakea katika Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro imetambuliwa huku mingine mitatu ikiwa bado haijatambuliwa. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amesema ajali…
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza kwa njia ya Simu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan alipopiga simu kuzungumza na wadau na Mashabiki wa mchezo wa ngumi, wakati wa tukio maalum la pambano la ngumi la ‘Knockout ya Mama’ linalofanyika katika ukumbi wa Super Dome, Masaki jijini Dar es…
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe Mwanaidi Ali Khamis amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan anawajali watu wenye Mahitaji Maalum kwani ameweka mazingira mazuri ya kuwalinda na kuwapatia huduma muhimu hasa katika Makao ya Watoto na Makazi ya Wazee yaliyopo nchini. Naibu…
Takwimu zikionyesha kuwa China ndiyo mbia namba moja wa biashara na uwekezaji nchini, kumekuwa na mchanganyiko wa mawazo juu ya wingi wa raia Taifa hilo namba mbili kwa uchumi duniani. Wapo wanaoona wingi wa Wachina nchini ni fursa ya maendeleo kwa kuongeza shughuli za kiuchumi na wengine wakihofu kuibuka kwa unyonyaji mpya wa uchumi na…
Malinyi. Wanakijiji wa Ngombo, wilayani Malinyi mkoani Morogoro wameilalamikia Serikali kwa kuanzisha oparesheni ya kuwaondoa katika kijiji hicho kupisha Pori la Akiba la Kilombero, bila kuwapatia eneo mbadala la kuhamia. Wanakijiji hao, walioko katikati ya Bonde la Kilombero, wamekubali kuondoka lakini wanahoji; wataenda wapi? Mkazi wa kijiji hicho, David Mkumba amesema alizaliwa Ngombo, na wazazi…
Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) imetupilia mbali rufaa ya Guinea dhidi ya Tanzania na hivyo kuipa uhakika Taifa Stars kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon 2025) nchini Morocco. Guinea ilikata rufaa hiyo baada ya mchezo namba 143 wa kuwania kufuzu Afcon baina yao na Tanzania uliochezwa katika Uwanja…
Dar/ Mikoani. Wakati Watanzania wakiungana na Wakristo duniani kote kuadhimisha Sikukuu ya Krismasi hali ya amani imetawala nchini jana, huku tukio la mauaji ya mfugaji na mkazi wa Lubungo wa Mvomero mkoani Morogoro, Elisha Lengai (20) likitia doa. Lengai anadaiwa kuchomwa kisu na Sikonye Kipondo (22) baada ya kutokea ugomvi ambao chanzo chake bado hakijafahamika….
Handeni. Unaweza kusema Desemba hii ni ya majonzi na simanzi kubwa kutokana na mfululizo wa ajali mbaya zilizotokea, zikiwamo zilizotokea jana wilayani Handeni Mkoa wa Tanga na nyingine iliyotokea leo Wilaya ya Rombo, mkoani Kilimanjaro ambazo zimesababisha vifo vya watu 20. Mwezi huu ambao kwa kawaida huwa wa shamrashamra za sikukuu za mwisho wa mwaka,…
Dodoma. Utata umegubika tukio la mauaji ya Graison Kenyenye (6), mtoto wa mfanyabiashara maarufu wa jijini Dodoma, Zainab Shaban maarufu Jojo. Graison aliuawa usiku wa kuamkia juzi, wakati mama yake alipokwenda matembezini na rafiki yake wa kiume. Tukio hilo lilitokea Ilazo Extension jijini Dodoma, usiku wa kuamkia Desemba 25, 2024, wakati Jojo alipomuacha mtoto huyo…