
KONA YA FYATU MFYATUZI: Wabongo tunarogwa na dini zetu wenyewe
Nimekuwa nikiepuka kuzifyatua dini, hasa kinachoendelea, hasara, maudhi, maangamizi, utapeli na wizi wa waziwazi yanayoanza kuzoeleka, nimelazimika kufyatuka na kufyatua vinavyoonekana kutofyatuliwa. Walipokuja wakoloni wa kitasha na wafanya biashara ya utumwa wa kimanga, walituletea dini na utamaduni wao, baada ya kuharibikiwa kwao wakatuharibu tukaharibikiwa. Kwanza, walifyatua dini zetu kwa kuzitukana, kuzidhalilisha na kuzizika, huku nasi,…