Mbowe ataka saa 48 kuamua hatima yake Chadema

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amewaomba viongozi, wanachama na makada waliofika nyumbani kwake kuwa wampe saa 48 za kutafakari ombi lao la kumtaka kuwania nafasi hiyo. Pia, amewaeleza kuwa hataingia kwenye vita itakayokibomoa chama hicho bali ataingia kwenye vita itakayokijenga. Mbowe ameyasema hayo leo Jumatano, Desemba 18, 2024 wakati akizungumza na wanachama…

Read More

Filamu ya Tantalizing Tanzania yazinduliwa rasmi nchini India

Filamu ya kutangaza vivutio vya utalii vya nchini Tanzania ijulikanayo kama “Tantalizing Tanzania” inayomhusisha mwanamuziki wa India Shakti Mohan aliyepiga picha mjongeo katika hifadhi za Serengeti, Ngorongoro na Zanzibar imezinduliwa nchini India. Filamu hiyo iliyoandaliwa na Kampuni ya Swahili iliyopo Mumbai nchini India imezinduliwa rasmi na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi…

Read More

Mbowe alivyotoka kuwahutubia wafuasi wake nyumbani

Dar es Salaam. Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamekusanyika nyumbani kwa Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, Mikocheni jijini Dar es Salaam kwa lengo la kumshawishi achukue fomu kuwania tena nafasi hiyo. Wafuasi hao wakiwa na shangwe na hamasa, wamefanya hivyo kama ishara ya kumuunga mkono, wakimsihi aendelee kuongoza chama hicho. Makamu…

Read More

Rais Samia na Dr. Leakey kutunukiwa Tuzo Arusha

Tanzania inatarajia kuzindua Tuzo za Kitaifa za Utalii na Uhifadhi Desemba 20, 2024, ikiwa ni hatua ya kutambua na kuenzi mchango wa wadau wa sekta hizo. Rais Samia Suluhu Hassan atatunukiwa tuzo ya heshima kwa mchango wake kupitia filamu za Royal Tour na Amazing Tanzania. Dk. Louis Leakey na Mary Leakey pia watatuzwa kwa uvumbuzi…

Read More

Ugonjwa wa Mpox wazidi kuenea Burundi – DW – 18.12.2024

Mkurugenzi wa kituo cha kukabiliana na magonjwa yanayoambukia Daktari Nyandwi Joseph anasema kamati ya kukabiliana na Mpox tayari imechapisha kitabu kinakachoonesha dalili za ungonjwa huo, kinga, na matibabu yake. Kitabu hicho kitaenezwa hivi karibuni katika hospitali, zahanati na shule pamoja na sehemu nyingine za umma Burundi. Tangu kuripotiwa mripuko wa ugonjwa huo unaosababishwa na virusi…

Read More

Hekaheka kimbunga Chido kikiacha balaa Mayotte, Msumbiji

Dar es Salaam. Watu 34 wameripotiwa kufariki dunia Msumbiji baada ya Kimbunga kilichopewa jina la Chido kuipiga nchi hiyo. Mbali na maafa hayo, inaelezwa hadi kufikia jana Desemba 17, 2024, jumla ya watu 174,158 wameathiriwa wameathiriwa namna mbalimbali na wengine 319 kujeruhiwa. Kimbunga hicho kiliipiga Msumbiji tangu Jumapili, Shirika la Umoja wa Mataifa la misaada…

Read More