Youssouf ashinda uenyekiti AU, Raila ashindwa

Mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), Mahmoud Youssouf wa Djibouti ameshinda nafasi hiyo. Mahmoud Youssouf ameshinda nafasi hiyo kwa kupata kura 33. Wagombea wengine walikuwa Raila Odinga wa Kenya na Richard Randriamandrato kutoka Madagascar. Odinga alikuwa akiwania nafasi hiyo na wagombea wengine ili kumpata atakayemrithi Moussa Faki Mohamed, Waziri…

Read More

Serikali yawaita kazini watumishi wapya 600, majina haya hapa

Dar es Salaam. Serikali imewaita watumishi zaidi ya 600 wa kada mbalimbali kuripoti kazini katika muda ambao utakuwa umepangwa katika barua za ajira watakazopewa. Majibu yaliyotolewa ni ya wale ambao waliofanya usaili kati ya Septemba 2, 2024 na Januari 17, 2024 na kufaulu ambayo yameunganishwa na mengine kutoka kanzidata. Taarifa kwa umma iliyotolewa na Sekretarieti…

Read More

Rais Tshisekedi akatisha ziara Ujerumani ‘kuiwahi nchi’

Kinshasa. Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Felix Tshisekedi amelazimika kukatisha ziara yake nchini Ujerumani, baada ya waasi wa M23 kuteka maeneo muhimu mashariki mwa nchi hiyo. Rais Tshisekedi alikuwa Munich nchini Ujerumani akihudhuria mkutano wa usalama ulioanza Ijumaa Februari 14 jijini humo. Taarifa ya Ofisi ya Rais Kinshasa DRC ilisema Rais Tshisekedi…

Read More

Makonda ataka wanaojenga kuwa na mpango wa kupanda miti

Arusha. Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda ameagiza mamlaka zinazohusika na kutoa vibali vya ujenzi ikiwemo mipango miji, kutokutoa vibali vya ujenzi kwa mtu atakayeomba kibali bila kuonyesha eneo atakalopanda miti ili kupunguza athari za mazingira. Ameagiza Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura) na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), kila wanapojenga barabara…

Read More

KenGold yaweka rekodi nyingine Bara

ACHANA na rekodi ya kuburuza mkia katika Ligi Kuu Bara tangu ilipoanza, sare ya bao 1-1 iliyoipata KenGold dhidi ya Tabora United juzi imeifanya kuandika rekodi ya kupata pointi kwa mara ya kwanza msimu huu ugenini, kwani kabla ya hapo ilikuwa haijashinda wala kutoka sare yoyote. Katika mchezo huo ambao KenGold ilitangulia kupata bao la…

Read More

Mtazamo wa wadau magari binafsi kulipia barabara ya BRT

Dar es Salaam. Wakati Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega akiwataka wataalamu wa sekta ya ujenzi kubuni mbinu za kupunguza foleni mijini, akipendekeza kutumiwa njia za Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) na magari binafsi kwa kulipia, baadhi ya wadau wameibua mtazamo tofauti. Ulega alitoa pendekezo hilo Februari 13, 2025 kwenye mkutano wa baraza la wafanyakazi wa wizara…

Read More