Wanaotoa mikopo umiza ujumbe wenu huu hapa

Geita. Serikali imezitaka kamati za ulinzi na usalama kuwachukulia hatua kali wale wanaotoa mikopo bila kuwa na leseni, pamoja na kuwanyang’anya leseni hizo wote wanaotoa mikopo bila kuzingatia masharti na kuwaumiza wananchi. Mikopo hiyo, ambayo imepachikwa majina mengi ikiwemo kausha damu, komandoo, pasua moyo, kichefuchefu na mengine mengi, imekuwa ikitajwa kuwa chanzo cha kufilisika, kujiua,…

Read More

Chunya kuzalisha kilo milioni 31 za tumbaku 

Mbeya. Jumla ya kilo milioni 31 za tumbaku zinatarajia kuzalishwa mkoani hapa  kwa msimu wa kilimo 2025/26 sambamba na uanzishaji wa mfuko wa majanga kwa wakulima. Uzalishaji huo umetajwa kuongezeka kutoka wastani wa kilo milioni 19 zilizopatikana msimu wa kilimo 2024/25 kati ya kilo milioni 26 zilizotarajiwa kuzalishwa. Akizungumza na Mwananchi leo Jumatatu, Februari 17,…

Read More

Upelelezi kesi ya kumiliki mijusi 226 bado

Dar es Salaam. Upelelezi wa kesi mbili za kumiliki mijusi 226 aina ya Coud Gecko yenye thamani ya Sh13.8milioni, inayomkabili mfanyabiashara, Hika Shabani Hika (48) maarufu Majoka na Shaban Salum Mzomoke (45) maarufu kama Kisukari, haujakamilika. Wakili wa Serikali, Frank Rimoy ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo Februari 17, 2025 wakati kesi hizo zilipoitwa…

Read More

Matumizi ya drone kuongeza uzalishaji wa pamba Maswa

Maswa. Matumizi ya teknolojia ya kisasa ya ndege zisizo na rubani (drone) katika kunyunyizia dawa kwenye zao la pamba yanatarajiwa kuongeza uzalishaji kutoka tani 13 katika msimu wa mwaka 2023/2024 hadi tani 50 katika msimu wa mwaka 2024/2025. Hayo yameelezwa leo, Februari 17, 2025, na Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Aswege Kaminyoge, katika Kijiji cha…

Read More

Bodi ya mikopo yavuna faida Sh1.5 trilioni ndani ya miaka 20

Dar es Salaam. Zaidi ya Sh1.5 trilioni imetengenezwa kama faida na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kupitia mikopo ya Sh8.2 trilioni iliyotolewa kwa wanafunzi. Faida hiyo imepatikana kupitia mikopo iliyowanufaisha zaidi ya wanafunzi 830,000 waliosoma katika ngazi mbalimbali ndani ya miaka 20. Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wakati wa kilele…

Read More

Daraja linalounganisha Tabora, Shinyanga kuondoa kero

Kahama. Ujenzi wa daraja linalounganisha mikoa ya Shinyanga na Tabora katika Mto Kasenga linatajwa kuwa suluhisho la usafiri na kuondoa kero kwa wananchi wa mikoa hiyo. Hayo yameelezwa na Mhandisi wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) Mkoa wa Shinyanga, Evans Maridai leo Februari 17, 2025 akisema kwa sasa upasuaji wa miamba umekamilika. “Daraja hili lina…

Read More

Tanzania itakavyopunguza foleni katika miji na majiji

Dodoma. Serikali imetangaza mpango mahususi wa kukabiliana na msongamano wa magari katika majiji matano na miji mitatu nchini ikiwamo upanuzi wa barabara zinazoingia katika maeneo hayo. Misururu ya magari imekuwa kawaida kuonekana asubuhi na jioni wakati watu wakielekea na kutoka kazini. Foleni zimekuwa ni za kawaida katikati ya majiji au miji inayokua. Kiafya, foleni pia…

Read More

Kicheko kwa wanaume wenye vipara

Wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Sheffield, Uingereza na wenzao kutoka Chuo Kikuu cha COMSATS nchini Pakistan, ndio waliogundua mafuta hayo. Kwa mujibu wa utafiti huo, mafuta yenye sukari (deoxyribose sugar) yana kemikali ya kaboni ambayo inasaidia kutokomeza upara. Wanasayansi waligundua hilo kibahati baada ya kuyapaka mafuta hayo kwenye sehemu ya mwili wa panya aliyekuwa amejeruhiwa…

Read More

Mapya Wapakistan wanaodaiwa kusafirisha dawa za kulevya

Dar es Salaam. Wakati Serikali ikiendelea na uchunguzi wa kesi ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya Heroine na Methamphetamine zenye uzito wa kilo 447.3 inayowakabili raia nane wa Pakistan, washtakiwa hao wamedai kuwa hawana nguo za kubadilisha huko gerezani. Pia, washtakiwa hao wamedai hawana mawasiliano na familia zao zilizopo Pakistan, tangu walipofikishwa mahakamani hapo….

Read More