Ndio, Ni kipindi ambacho hata waliokuwa wanaandamana walipoishiwa nguvu polisi waliwasaidia .Hiyo tumeshuhudia kwa Rais Samia tu katika uongozi wake.
Awamu ya Tano wapinzani hawakuwa na ujanja walikuwa kimya,hakuna mkutano wala maandamano.Hawakuthubutu na wengine walikimbia Nchi.
Hivyo wakati tunaadhimisha miaka minne ya Rais Samia Suluhu Hassan madarakani tunasema ahsante kwa kuja na R nne kwani zimeleta utulivu .
Hata wale waliokuwa wamekimbia nchi leo tunao,wanatamba tu huko mtaani.Wameshasahau yaliyowatokea.Watu bwana kweli tumeumbwa wa kusahau.
Rais Samia nakupongeza kwa uongozi wako katika miaka minne yako ajira mpya za kumwaga,wakati unachukua nchi ajira mpya zilikuwa 7000 lakini katika muda wa miaka minne umetoa ajira mpya 34000 na mikakati ya kuajiri zaidi imeendelea kuchukuliwa.
Nenda katika sekta ya afya ,bajeti ya dawa na vifaa tiba imeongezwa,ujenzi wa miundombinu ya Zahanati,Vituo vya afya na Hospitali za Rufaa zimejengwa katika kipindi cha miaka minne ya Rais Samia.Hongera Mama Super Women ,Mama Samia Mitano tena!
Kuna mengi yamefanywa na Rais Samia katika kipindi cha miaka minne, makusanyo ya kodi yameongezeka na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) inajivunia.
Kwa mfano tu katika kipindi cha Januari 1 mwaka huu wa 2025 TRA imevunja rekodi ya makusanyo tangu kuanzishwa kwake kwa kukusanya Sh.Trilioni 3.587 kwa mwezi Desemba.
Hivyo ukisikia Watanzania wanasema wana imani kubwa na Rais Samia Suluhu Hassan ni kwasababu anayofanya yanaonekana. Amefanya na anaendelea kufanya kwa ajili ya kubadilisha maisha ya Watanzania kutoka haya ya sasa na kuwa bora.
Katika miaka minne ya Rais Samia ametufundisha kuwa nchi inaweza kusonga mbele bila ya kuumiza wengine,anaamini katika haki,anaamini katika kujenga Taifa linaloishi kwa misingi ya kuheshimiana.
Lakini ngoja nikwambie tu katika sekta ya michezo unakumbuka goli la Mama ambavyo limeleta hamasa katika michezo na hasa mchezo wa soka.
Miaka minne ya uongozi wake timu za Simba na Yanga zimevuna mamilioni ya fedha. Goli la Mama limeleta chachu katika mpira wetu.
Hata hivyo Rais Samia ameweka nguvu katika michezo yote na kote huko amekuwa akitoa fedha kama sehemu ya kuhamasisha michezo. Hapo sijagusia ujenzi wa miundombunu ya viwanja vya michezo mbalimbali.
Miaka minne ya Rais Samia inaacha alama ya mbegu nzuri aliyoipanda katika sekta ya michezo.Tunakupongeza Rais Samia, wadau wa michezo wanathamini na kuheshimu jitihada zako…
Pamoja na yote hayo nikiri Rais Samia anaongozwa na Utu,uwajibikaji,uwezo,uvumilivu,uzalendo na ushawishi.Hakika watanzania tunajivunia uongozi wa Rais Samia,upendo wake kwetu hauna hata chembe ya shaka.Rais Samia katika miaka minne ametuonesha upendo wa kweli.
Hata hivyo nihitimishe kwa kusema tu katika miaka minne ya uongozi wa Rais Samia bila kujali anapitia changamoto gani uso wake muda wote umejaa tabasamu,uso umejaa nuru inayoangaza maisha ya Watanzania.
Jicho lake sasa,linaona wema na wabaya lakini cha kufurahisha alishasema Ukizingua atakuzingua….Mama Samia Super Women,Mama Samia mitano tena.
Kwa haya ambayo Rais Samia ameyafanya katika miaka minne amejikuta amekuwa kipenzi cha Watanzania,wanamsubiria tu katika uchaguzi mkuu wampe kura halafu iwe Mitano Tena…
Watanzania wanasubiria tu tarehe ya Uchaguzi Mkuu itangazwe na wakati ukifika wachukue, waweke Waaa…habari ya No Reform No Election wanaona kama haiwahusu vile, Ni kauli ya blaza na ndugu zake.Imeisha hiyoooo ,ni MAMA SAMIA TU, Wengine mbwembwe tu.
Simu 0713833822/0762451570.