Aliyebuni jina ‘Tanzania’ afariki dunia

Dar es Salaam. Mohammed Iqbal Dar mbunifu wa jina la Tanzania, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80 jijini Birmingham, Uingereza, ambako aliishi tangu ahamie mwaka 1965. Kifo chake kimetokea baada ya kuugua kwa muda wa miaka takriban 10, ambapo alikuwa hawezi kutembea akiwa chini ya uangalizi wa karibu nyumbani. Mohammed Iqbal Dar alizaliwa…

Read More

TBF yaanza na vijana wapya 45

VIJANA 45 wanaocheza kikapu wenye umri wa miaka 16-18 wameshiriki katika kliniki ya mchujo wa kutafuta timu ya taifa ya vijana kwenye Uwanja wa Donbosco, Oysterbay, Dar es Salaam. Kliniki hiyo iliandaliwa na Shirikisho la Kikapu Tanzania (TBF), ikiwa chini ya udhamini na ICARRe Foundation, ambapo Mwanaspoti lililokuwepo uwanjani hapo lilishuhudia vijana hao wakianza kwa…

Read More

Madaktari watoa taarifa mpya hali ya Papa Francis

Rome, Vatican. Hali ya kiafya ya Kiongozi wa Kanisa Katoliki, Papa Francis, imeendelea kuwa ya wasiwasi baada ya kushindwa kupumua kutokana na makohozi kuziba njia za hewa. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Vatican, madaktari walilazimika kutumia mashine kuondoa makohozi hayo na kumuweka tena kwenye mashine ya kumsaidia kupumua. Hata hivyo, licha ya hali…

Read More

Saratani kwa wasiovuta sigara yaongezeka – utafiti

Dar es Salaam. Utafiti mpya uliotolewa na taasisi ya saratani ya Shirika la Afya Duniani (WHO) umeonyesha kuwapo kwa ongezeko la wagonjwa wa saratani ya mapafu kwa watu ambao hawajawahi kuvuta sigara, wanawake wakiongezeka zaidi. Matokeo ya utafiti huo yaliyochapishwa na jarida la The Lancet Respiratory Medicine yanaonyesha saratani ya adenocarcinoma, aina ya saratani ya…

Read More

Aziz KI ana kitu cha kufanya Dabi ya Kariakoo

Kiungo wa Yanga, Stephane Aziz Ki ametoa ahadi ya kumpa zawadi, Waziri wa Madini na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini la Klabu hiyo, Anthony Mavunde katika siku ya mchezo wao dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Machi 8 mwaka huu kuanzia saa 1:15 usiku. Hilo sio jambo geni kwa Stephane Aziz Ki kwani…

Read More

Trump asitisha msaada wa kijeshi kwa Ukraine

Washington. Rais wa Marekani, Donald Trump, ameagiza kusitishwa kwa msaada wote wa kijeshi kwa Ukraine siku chache baada ya mvutano mkali kati yake na Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, katika Ikulu ya White House. Hatua hiyo imekuja baada ya mkutano wa faragha kati ya viongozi hao wawili, ambapo Trump anadaiwa kumpa Zelensky sharti la kukubali…

Read More

Tiba asili zinavyoweza kuharibu figo zako

Dar es Salaam. Kama wewe ni miongoni mwa watumiaji wa tiba asili, unapaswa kujua kwamba unaziweka hatarini figo zako. Hii ni kutokana na dawa nyingi za asili kutopitia mchakato wa kupimwa viwandani na kutoa majibu ni kiwango gani unapaswa kukitumia kujitibu, ambacho mwili unaweza kumudu au kustahimili nguvu ya dawa. Hayo yameelezwa na daktari mbobezi…

Read More