Polisi watoa onyo kwa waganga wanaowakata vimeo watoto

Morogoro. Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limetoa onyo kali kwa waganga wanaoshiriki vitendo vya kikatili dhidi ya watoto, ikiwamo kukata vimeo, kung’oa meno na kukata ngozi ya chini ya ulimi (udata), kwa madai ya vitendo hivyo ni vya kinyume na sheria na vinakiuka haki za watoto. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi…

Read More

Bugando kuanza upandikizaji figo mwaka huu

Mwanza. Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando imesema inatarajia kuanza kutoa huduma ya upandikizaji wa figo kwa wagonjwa wanaofanyiwa huduma ya usafishaji damu (Dialysis) mwaka huu. Taarifa hiyo imetolewa leo Alhamisi, Machi 13, 2025, na Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji Bugando, Dk Alicia Masenga, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Bugando,…

Read More

Jela maisha kwa kulawiti mtoto wa miaka 12 Mufindi

Mufindi. Mahakama ya Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, imemuhukumu kifungo cha maisha jela mkazi wa kijiji cha Ibatu Kata ya Igowole Tarafa ya Kasanga, Michael John Ngunda (27) baada ya kumtia hatiani  kwa kosa la kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka (12). Hukumu hiyo imetolewa jana Machi 12, 2025 na Hakimu Mkazi Sekela…

Read More

PIC yaridhishwa na utekelezaji wa mradi wa HEET Udom

Dodoma. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC) imesema imeridhishwa na utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa maabara za sayansi na madarasa ya masomo ya kada ya ardhi kwenye Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom). Mradi huo utakaowezesha kupanua wigo wa udahili wa wanafunzi kwenye chuo hicho, unatekelezwa chini ya Mradi…

Read More

Songamnara, Kilwa kisiwani kinara kuvutia watalii

Kilwa. Mamlaka ya wanyamapori Tanzania (Tawa) imeyataja maeneo ya Songamnara na Kilwa kisiwani kuwa kinara kwa kutembelewa na watalii mkoani Lindi. Hayo yamesemwa Machi 12, 2025 na Kamishna Msaidizi wa uhifadhi Kanda ya Kusini Mashariki, Hadija Malongo akizungumza wakati wa kuwapokea watalii katika eneo la Songamnara. Hadija amesema kuwa hadi sasa Tawa wameshapokea watalii zaidi…

Read More

Mchengerwa ampa siku 60 mkandarasi kumaliza ujenzi

Dodoma. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa, amempa miezi miwili (sawa na siku 60) mkandarasi wa jengo la Tamisemi kukamilisha ujenzi baada ya kuchelewa kwa zaidi ya mwaka mmoja. Ujenzi wa jengo hilo lenye ghorofa sita, litakalokuwa na uwezo wa kuchukua wafanyakazi 600, ulianza…

Read More

Tahadhari kukabili Mpox, Serikali yatoa muongozo

Unguja. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeeleza mikakati inayochukua kukabiliana na ugonjwa wa homa ya nyani (Mpox) ikiwa ni pamoja na ufuatiliaji wa magonjwa katika vituo vya afya na upimaji wasafiri wanaoingia kwenye visiwa hivyo. Machi 10,2025 Wizara ya Afya Tanzania Bara ilithibitisha uwapo wa wagonjwa wawili wenye maambukizi ya ugonjwa huo. Hata hivyo,…

Read More

Presha juu ugawaji majimbo | Mwananchi

Dar/ mikoani. Joto la Uchaguzi Mkuu mwaka huu limezidi kupanda na kukoleza maombi ya kugawa maeneo ya uchaguzi ambayo hadi sasa yameyagusa takriban majimbo 14. Mchakato huo ni kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, inayoipa mamlaka Tume Huru ya Uchaguzi (INEC) kugawa mipaka ya majimbo ya uchaguzi. Presha hiyo ilianza kupanda ndani ya vyama, hasa…

Read More