WAKATI umesalia muda mfupi kabla ya mchezo wa robo fainali ya pili kupigwa, hali ya hewa ya mvua iliyoanza kunyesha mapema leo imeleta changamoto katika maandalizi ya mchezo huo.
Katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, juhudi kubwa zinaendelea kuondoa maji kwa uchache yaliyotuama kwenye baadhi ya maeneo ya kuchezea.
Watu wanaoonekana kuwa na utambulisho maalum kwa kuvaa bips wamejigawa maeneo tofauti ya uwanja huo. Kila kundi linafanya kazi kuhakikisha maji yanayotuama hayataathiri ubora wa mchezo unaosubiriwa kwa hamu.

Baadhi yao wanaonekana wakitumia magodoro madogo kujaribu kunyonya maji kwenye sehemu za nyasi ambazo zimeathirika zaidi.
Wengine, wakiwa na mifagio maalum ya kusukuma maji,