Wakati Simba ikijihakikishia kiasi cha Dola 750,000 kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kwa kufuzu nusu fainali ya kombe la Shirikisho Afrika, kocha mkuu wa timu hiyo Fadlu Davids amefichua mipango ya kumsajili kiungo bora mshambuliaji mzawa ambaye hata hivyo hajamtaja jina.
Ushindi wa mikwaju ya penalti 4-1 dhidi ya Al Masry jana baada ya sare ya mabao 2-2 katika mechi mbili za robo fainali, umeifanya Simba kutinga nusu fainali ambapo itakutana na Stellenbosch ya Afrika Kusini.
Kwa kuingia nusu fainali, Simba imejihakikishia kiasi cha Dola 750,000 (Sh2 bilioni) ambacho kila timu inayotinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika inakuwa na uhakika wa kuvuna kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
Timu inayoishia hatua ya nusu fainali inapata kiasi hicho cha fedha lakini Simba inaweza kupata kitita kikubwa zaidi iwapo itatinga fainali au kuchukua ubingwa wa mashindano hayo.
Kwa mujibu wa muongozo wa CAF wa mgawanyo wa fedha za zawadi za Kombe la Shirikisho Afrika, timu inayoshika nafasi ya pili katika mashindano hayo inapata kitita cha Dola 1 milioni (Sh2.7 bilioni) na bingwa anapata kiasi cha Dola 2 milioni (Sh5.4 bilioni).
Wakati ikiwa na uhakika wa fedha hi