Stam azitamani pointi za Yanga

KOCHA Msaidizi wa Fountain Gate, Amri Said ‘Stam’ amesema kikosi chao kimeanza kuonyesha matumaini na kutibu madhaifu yaliyokuwepo hivyo wako tayari kuzipambania alama tatu katika mchezo ujao wa Ligi Kuu dhidi ya Yanga.

Stam ambaye kwa sasa anasaidiana na Khalid Adam waliiongoza timu hiyo juzi kupata sare ya bao 1-1 na Pamba Jiji katika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza huku Kocha Mkuu, Robert Matano raia wa Kenya akikosekana kwenye benchi.