Straika Stellenbosch aingiwa ubaridi, adai Simba ni hatari

Kwa mara nyingine macho na masikio ya wapenda soka yataelekezwa Zanzibar, Jumapili hii, pale Simba  itakapoumana na Stellenbosch ya Afrika Kusini katika mchezo wa nusu fainali ya kwanza ya  Kombe la Shirikisho Afrika utakaopigwa kwenye Uwanja wa New Amaan Complex.

Katika kuelekea mchezo huo mshambuliaji wa Stellenbosch, Andre Ernest de Jong, raia wa New Zealand, amesema kikosi chao kimejiandaa kimwili na kiakili kuhakikisha kinapata matokeo chanya katika ardhi ya ugenini ili kuweka mazingira mazuri ya kutinga fainali kwenye mechi ya marudiano nyumbani, Afrika Kusini.

“Tuna furaha kubwa sana kucheza dhidi ya Simba,” amesema De Jong. 

“Tunatambua ni klabu kubwa barani Afrika na tumejifunza mengi katika hatua zilizopita, hasa tulipoikabili Zamalek.  Tumethibitisha kwamba tunaweza kupambana na vigogo wa bara hili, na malengo yetu ni kupata matokeo mazuri hapa Zanzibar kabla ya kurudiana nyumbani.”

Wakati wengi wakidhani kucheza nje ya Uwanja wa Benjamin Mkapa ni nafuu kwa wapinzani wa Simba, De Jong anaamini hakuna tofauti kwani wachezaji wa Simba wamezoea mazingira ya Tanzania kwa ujumla. 

Related Posts