By Ngilisho Tv-VATCAN
Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, amefariki dunia leo Jumatatu ya Pasaka, Aprili 21, 2025, akiwa na umri wa miaka 88. Taarifa rasmi kutoka Vatican zinaeleza kuwa Papa Francis amefariki akiwa nyumbani kwake katika makazi ya Casa Santa Marta, Vatican.
Papa Francis, aliyezaliwa mwaka 1936, amehudumu kama Papa tangu mwaka 2013 na alikuwa kiongozi wa kwanza wa Kanisa Katoliki kutoka Amerika ya Kusini.