KATI ya mashirikisho 54 ya soka Afrika ambayo yanapeleka timu zao kushiriki Ligi ya Mabingwa Afrika yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kila msimu, Tanzania tayari imepata mwakilishi wake mmoja, bado mwingine.
Kwa mujibu wa CAF, mashirikisho yaliyopo kwenye orodha ya 12 bora kwa viwango, yanawakilishwa na klabu mbili kwenye Ligi ya Mabingwa.
Kwa wastani, timu 68 zinatarajiwa kushiriki michuano hiyo, lakini tayari mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Yanga imejihakikishia tiketi moja kwa msimu ujao, baada ya kukusanya pointi 70 katika michezo yake 26 ya Ligi Kuu Bara ambazo haziwezi kuwatoa nafasi mbili za juu kwenye msimamo, hivyo moja kwa moja imefuzu.