KESI MGOGORO WA RASILIMALI CHADEMA: Mahakama yaipa Chadema siku 21 kuwasilisha utetezi
Dar es Salaam. Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam, imekipa siku 21 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwasilisha mahakamani utetezi wake wa maandishi katika kesi ya mgogoro wa mgawanyo wa rasilimali na uendeshaji, inayokikabili. Kwa maana hiyo chama hicho kimeamriwa kuwasilisha mahakamani hapo utetezi wake huo kabla au mpaka kufikia Mei 9, 2025….