Vituo 10 vya bunifu kujengwa kwa gharama ya Sh15 bilioni

Unguja. Katika kukuza na kuwaendeleza wabunifu wa kidijitali na wajasirimali, vinajengwa vituo 10 vya bunifu nchini vitakavyogharimu Sh15 bilioni. Kati ya hivyo, vinane vitakuwa ni vya kukuza ujasiriamali wa kutengeneza mifumo na viwili vitakuwa vinatumika kutengeneza vifaa. Vituo hivyo vinavyojengwa katika mikoa minane, mifumo yake itaunganishwa ili fursa zinazopatikana nchini, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)…

Read More

WANANCHI BABATI WALIA WIZI WA MIFUGO.

Na John Walter -Babati Wananchi wa Tarafa ya Mbugwe, wilayani Babati, mkoani Manyara, wameeleza kilio chao mbele ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Daniel Sillo, wakilalamikia wizi wa mifugo unaofanywa na watu wasiojulikana. Wazee wa jamii ya kifugaji wamesema kuwa wizi huo umekithiri katika tarafa hiyo, hali inayowaathiri kiuchumi na kuleta hofu…

Read More

UWEKEZAJI SAHIHI NA AKIBA ENDELEVU: NGUZO YA MAFANIKIO KWA WANANCHI WA MWANZA

Na Chedaiwe Msuya, WF, Mwanza. Serikali kupitia Wizara ya Fedha imeendelea kutoa  elimu ya fedha kwa wananchi wa makundi mbalimbali katika Mkoa wa Mwanza, hatua inayolenga kuwawezesha kujenga misingi imara ya kifedha kwa maendeleo endelevu.  Wajasiriamali wa Kata ya Misungwi, Wilaya ya Misungwi, Mkoa wa Mwanza, wameelezea shukrani zao kwa Serikali kwa kuwawezesha kupata elimu…

Read More

WANAKWAYA SITA WAFARIKI DUNIA WAKIENDA KUINJILISHA INJILI..

NA WILLIUM PAUL, SAME. WATU sita ambao ni Wanakwaya wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) usharika wa Chome wilayani Same mkoani Kilimanjaro, wamefariki dunia huku wengine 23 wakijeruhiwa baada gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali. Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Mwenyekiti wa ulinzi na usalama wilaya ya Same ambaye pia ni Mkuu wa wilaya…

Read More

Rais Mwinyi ahimiza amani kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba

Unguja. Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa kudumisha amani, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu. Amesema kila mmoja anapaswa kuiombea dua nchi ili mchakato wa uchaguzi mkuu upite kwa amani na mshikamano. Akizungumza leo Jumatatu, Machi 31, 2025, katika Baraza la Idd lililofanyika Polisi Ziwani, Unguja, baada…

Read More

Ukomo, elimu nafasi ya ubunge mjadala mzito

Moshi/Dar. Mjadala wa ukomo kwa nafasi ya ubunge wa jimbo, umeanza kupamba moto huku baadhi ya wasomi na wananchi wakiikumbuka Rasimu ya Katiba ya Tume ya Jaji Joseph Warioba iliyoweka ukomo wa miaka 15 katika nafasi hiyo. Wanaochagiza uwepo wa ukomo, wanaenda mbali na kutaka pia kuwepo kwa kiwango cha chini cha elimu kutokana na…

Read More