Mabao 10 ya Msuva na maana yake

MABAO 10 aliyofunga mshambuliaji wa Kitanzania, Simon Msuva kwenye klabu ya Al Talaba yameifanya timu hiyo kusalia nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi. Hadi sasa Ligi ya Iraq zimebaki mechi tano kumaliza msimu 2024/25, chama la Mtanzania huyo likiwa nafasi ya nne kwenye mechi 27, baada ya kushinda mechi 14, sare tano na kupoteza…

Read More

Chama la Wana lazipotezea 8-1 za Yanga

LICHA ya Stand United ‘Chama la Wana’, kuchapwa kwa mabao 8-1, dhidi ya Yanga katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho (FA), kocha wa kikosi hicho, Juma Masoud amesema kichapo hicho hakijawaharibia malengo yao ya msimu huu. Akizungumza na Mwanaspoti, Masoud alisema licha ya kuruhusu mabao mengi alikaa na wachezaji na kuwataka kusahau…

Read More

Fredrick Magata bado pointi tatu tu

KIUNGO mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Fredrick Magata anasubiri kwa hamu kuandika historia tamu ya maisha yake kwa kuhusika katika kuzipandisha Ligi Kuu Bara timu mbili tofauti. Timu yake ya sasa, Mtibwa imebakisha pointi tatu tu kurejea Ligi Kuu msimu ujao, jambo ambalo litakuwa ni mara ya pili kwa nyota huyo baada ya msimu wa 2021-22…

Read More

CUF, ACT-Wazalendo wanavyowang’atia G55 | Mwananchi

Dar es Salaam. Imebaki kwa G55, kuamua ni jukwaa gani la kisiasa wanaweza kulitumia ili kutimiza malengo yao ya kugombea nafasi za ubunge, baada ya Chama cha Wananchi (CUF), kuungana na vyama vingine kuwakaribisha. G55 ni kundi la wananchama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wanaopingana hadharani na msimamo wa chama hicho wa kuzuia…

Read More

Viongozi wa Serikali waonya vurugu za uchaguzi

Dar/Mikoani. Viongozi wakuu wa nchi katika ujumbe wao wa Pasaka, wamezungumzia uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, wakiwataka wananchi kujitokeza kushiriki na kuepuka vurugu. Mbali na hayo, wamewakataka kutafakari kuhusu upendo, haki na wajibu. Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango ametoa rai kwa wazazi, hususani kina mama kuwaongoza watoto wao, hasa vijana kuacha tabia ya…

Read More

Utitiri wa malori janga kwa barabara

Dar es Salaam. Ingawa kuharibika mara kwa mara kwa miundombinu ya barabara kunachochewa na sababu nyingi, kukosekana udhibiti wa malori ya mizigo yanayopita kwenye barabara hizo inatajwa kuwa sababu kuu. Kwa mujibu wa wadau wa miundombinu hiyo, barabara hujengwa kwa kuzingatia aina na uzito wa vyombo vya usafiri vinavyokusudiwa kupita na kitendo cha kuruhusu lori…

Read More

Viongozi wa dini washusha nondo kuelekea uchaguzi

Dar/Mikoani. Ikiwa imesalia takribani miezi sita Tanzania kuingia katika uchaguzi mkuu, viongozi wa dini wametoa wito kwa Serikali na wadau wa siasa kuhakikisha unakuwa huru na wa haki, wakisisitiza kuwapo mabadiliko ya mifumo kabla ya uchaguzi, huku wanaoshikiliwa waachiwe huru pasipo masharti. Kwa nyakati tofauti wakihubiri wakati wa mkesha wa Pasaka, Aprili 19 na sikukuu…

Read More

Julietha Singano anazidi kung’ara Mexico

BEKI wa kimataifa wa Tanzania, Julietha Singano anazidi kuwakosha mashabiki wa FC Juarez inayoshiriki Ligi ya Wanawake nchini Mexico baada ya juzi kuingia kwenye kikosi bora cha wiki. Huu ni msimu wa tatu mfululizo kwa beki huyo wa timu ya taifa ‘Twiga Stars’ kuichezea timu hiyo akifanikiwa kuingia kwenye kikosi cha kwanza moja kwa moja…

Read More

Waliofariki ajalini Iringa kuagwa kesho

Mafinga. Miili ya watu sita kati ya saba waliofariki dunia katika ajali ya gari la kubebea wagonjwa lililogongana na pikipiki ya magurudumu matatu, maarufu ‘Guta’ inatarajiwa kuagwa kesho Jumatatu Aprili 21, 2025. Inaagwa miili sita, kwa sababu mmoja tayari umeshatambuliwa na kuchukuliwa na ndugu zake. Ajali hiyo ilitokea Aprili 19, 2025, saa 12:30 asubuhi katika…

Read More