Tuzo za umahiri sasa kutolewa Zanzibar

Unguja. Kwa mara ya kwanza Zanzibar imeandaa tuzo za umahiri katika mawasiliano ambazo zitashirikisha waandishi wa habari kutoka ndani na nje ya nchi. Tuzo hizo ambazo zimeandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar, Taasisi ya Uhusiano ya Umma Tanzania (IPRT) na Idara ya Habari Maelezo Zanzibar, zinatarajiwa kutolewa Julai 5 mwaka huu kisiwani humu….

Read More

RC atishia kufunga biashara kisa uchafu

Pemba. Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid amesema Serikali ya Mkoa huo itachukua hatua za kisheria dhidi ya wafanyabiashara watakaoshindwa kudumisha usafi katika maeneo yao ya kazi, ikiwemo kufungia biashara zao. Kauli hiyo ameitoa leo Ijumaa Aprili 18, 2025, wakati wa operesheni maalum ya usafi wa mazingira iliyofanyika katika maeneo mbalimbali ya…

Read More

Masheha, watendaji walaumiana uchimbaji holela mchanga, mawe

Unguja.  Wakati Wizara ya Maji, Madini na Maliasili Zanzibar ikidai masheha ndio wanawajibika kulinda mali zisizohamishika, wao wamesema baadhi ya watendaji wa wizara ndio wanaoshirikiana na watu wanaofanya uharibifu huo.  Kwa mujibu wa sheria ya mazingira ya mwaka 2015, utartibu wa kuchimba mchanga, mawe na kuvisafirisha vinatakiwa kuombewa kibali maalumu wizarani huku yakitengwa maeneo maalumu ya…

Read More

Haki, amani vyatawala ibada ya Ijumaa Kuu Arusha

Arusha. Amani ya Tanzania ili iendelee kudumu, viongozi wa Serikali wametakiwa kuongeza kiwango cha uvumilivu na kuepuka matumizi ya nguvu kupita kiasi kwa baadhi ya watu wenye mitazamo tofauti. Aidha, wametakiwa kutenda haki kwa watu wanaowaongoza, na pale wanapotofautiana kujenga tabia ya kutumia njia ya mazungumzo kwa ajili ya kumaliza tofauti zao. Wito huo umetolewa…

Read More

Ambundo ajichomoa Fountain Gate | Mwanaspoti

KIUNGO mshambuliaji wa Fountain Gate, Dickson Ambundo amejiengua katika kikosi hicho kwa madai ya kutolipwa malimbikizo ya fedha zikiwamo za usajili zipatazo Sh50 milioni. Ambundo alijiunga na Fountain Gate mwanzoni mwa msimu huu akitokea Singida Black Stars na ameifungia timu hiyo mabao mawili kabla ya kuondoka kambini wakati timu ikipambana kumaliza katika nafasi nzuri katika…

Read More

Kocha Azam FC bado hajatupa taulo Bara

KOCHA Mkuu wa Azam FC, Rachid Taoussi amesema bado hajakata tamaa ya kupambana kumaliza ndani ya Nne Bora ya Ligi Kuu na kwa sasa anarejea tena katika vita ya ligi hiyo kwa kukabiliana na Kagera Sugar ugenini ili kujiweka pazuri. Azam itakuwa kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Kagera kukabiliana na wenyeji, ikiwa imetoka kupoteza mechi…

Read More

Huu hapa mtihani wa Kibu Denis katikati ya Waarabu

MICHUANO ya Kombe la Shirikisho Afrika ipo hatua ya nusu fainali ambazo zinapigwa kesho Jumapili, wakati Simba itakapokuwa wenyeji wa Stellenbosch ya Afrika Kusini na CS Constantine ya Algeria itakuwa wageni wa RS Berkane ya Morocco. Timu hizo zitarudiana wikiendi ijayo kusaka timu mbili za kwenda fainali. Lakini sasa, hadi kufikia hatua hiyo kiungo mshambuliaji…

Read More

JKT yaeleza sababu ya kuanzisha bustani za wanyamapori

Kibaha. Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele amesema kuanzishwa kwa bustani za wanyama ndani ya kambi za jeshi hilo ni sehemu ya kuongeza vyanzo vya mapato vinavyoweza kuboresha huduma mbalimbali na kupanua wigo wa ajira. Baadhi ya kambi za jeshi hilo ambazo tayari zimeanzisha bustani za wanyama ni Mbweni iliyopo…

Read More