Timu ya Soka ya Chuo Cha Uhasibu Arusha (IAA SC) imetwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Mikoa RCL 2025 baada ya kuifunga Misitu ya Tanga kwa penalti 4-2 katika mchezo wa fainali baada ya dakika 120 kumalizika kwa sare ya 2-2.
IAA sasa imeongeza idadi za timu za Arusha katika mashindano makubwa ambayo yanasimamiwa na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kufikia tatu, awali zilikuwa mbili Mbuni na TMA Stars ambazo ziko Ligi ya Championship na sasa pia IAA ya ambayo imepanda First League.
Katika mechi hiyo ya fainali iliyopigwa leo Ijumaa Mei 2, 2025 kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo jijini Arusha ambapo dakika 45 za kwanza zilianza kasi huku IAA wakimiliki mchezo kwa asilimia kubwa.
Ambayo iliwafaidisha dakika ya 23 kupitia Jeremia Ephu aliyefunga kwa penalti baada ya kipa wa Misitu kumfanyia madhambi mchezaji wa IAA.
Kipindi cha pili, Misitu walirejea kwa kasi na kuchukua mechi hiyo wakitaka kurekebisha makosa walifanya kipindi cha kwanza lakini kukosa umakini kwa safu ya ushambuliaji na umakini wa mabeki wa IAA .
Iliwachukua hadi dakika ya 90+4 Msitu kuwakatili wakati vijana wa Chuo cha Uhasibu Arusha waliokuwa wanaamini tayari wameshatwaa ubingwa kwa kufunga bao la kusawazisha.
Kwa mujibu wa kanuni ya mashindano ya RCL hatua ya fainali na mshindi wa tatu dakika 90 zik