Sh200 milioni zatekeleza miradi ya kijamii Buziba

Geita. Mgodi wa dhahabu wa Mwamba uliopo katika Kijiji cha Buziba, Kata ya Nyarugusu, Wilaya ya Geita umetumia zaidi ya Sh200 milioni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kijamii ikiwemo ya elimu na afya. Utekelezaji wa miradi hiyo ni sehemu ya mpango wake wa kurejesha kwa jamii, faida ya rasilimali zinazochimbwa kwenye maeneo yao….

Read More

Rais Mwinyi aahidi mamilioni Simba ikitwaa ubingwa CAFCC

Unguja. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameahidi kuizawadia Klabu ya Simba, Dola  za Marekani 100, 000 (Sh269 milioni) endapo itafanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika. Mechi ya Simba dhidi ya Berkane ya Morocco inatarajiwa kuchezwa kesho Jumapili saa 10: 00 jioni katika…

Read More

UVCCM yahamasishana kujiandikisha kupiga kura

Dodoma. Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), umewataka wapiga kura wapya kuwahamasisha vijana wengine kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura ili kushiriki ipasavyo kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka 2025. Kauli hiyo imetolewa huku kukiwa na changamoto ya idadi ndogo ya wapiga kura waliojitokeza katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 28,2020. Katika uchaguzi mkuu…

Read More

Mbeki ataka ukweli kwa viongozi wa Afrika

Dar es Salaam. Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki amewataka viongozi wa Bara la Afrika kuwa wakweli na waaminifu katika kulinda masilahi ya bara lao, ili kufanikisha malengo ya kukuza uchumi na kuboresha maisha ya Waafrika. Mbeki ameyasema hayo katika hafla ya chakula cha jioni iliyofanyika Mei 23, 2025 jijini Dar es Salaam. Mbeki…

Read More

Bei lita moja maziwa ya nyuki yagonga Sh12 milioni

Moshi. Wafugaji wa nyuki mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuchangamkia fursa za kiuchumi zitokanazo na mazao ya nyuki ikiwemo maziwa na asali ambapo bei ya lita moja ya maziwa ya nyuki inafikia takribani Sh12 milioni katika soko la kimataifa. Tanzania inatajwa kuwa nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali duniani, ikizalisha takribani tani 38,000 kwa mwaka, ikitanguliwa…

Read More

Othman aanza ziara Kanda ya Ziwa, aamsha ari ya mageuzi

Shinyanga. Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Taifa, Othman Masoud Othman, amewahimiza wananchi wa Shinyanga kutafakari kwa kina kuhusu mchango wao katika kuleta mageuzi. Amewakumbusha kuwa kila kura ina thamani kubwa na ni silaha muhimu ya kuleta mabadiliko ya kweli. Akizungumza leo Jumamosi, Mei 24, 2025, katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Town School,…

Read More

Operesheni C4C ya Chaumma yasogezwa mbele hadi Juni Mosi

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Salum Mwalimu ametangaza kusogezwa mbele kwa operesheni yao ya C4C (Chaumma For Change) ambapo sasa itazinduliwa Juni Mosi, 2025 jijini Mwanza badala ya Mei 30, 2025 iliyotangazwa awali. Operesheni hiyo ya Chaumma, itakayofanyika kwa kutumia chopa, ina lengo la kuimarisha chama hicho na…

Read More

Hifadhi ya Saanane yavuna Sh1.4 bilioni kwa miaka saba

Mwanza. Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Saanane imekusanya zaidi ya Sh1.4 bilioni kutoka kwa watalii 123, 292 waliotemelea hifadhi hiyo kwa takriban miaka saba iliyopita, ikiwa ni wastani wa zaidi ya watalii 17,000 kwa kila mwaka. Katika kipindi hicho, jumla ya watalii 119,532 kutoka Mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) walitembelea hifadhi hiyo…

Read More