Waliokata nguzo ya Tanesco wakidai kutumwa na Mungu watupwa jela
Mufindi. Mahakama ya Wilaya ya Mufindi imewatia hatiani wanandugu watatu, katika kesi ya jinai, waliokuwa wakikabiliwa na shtaka la uharibifu wa mali kwa kuvunja nguzo ya umeme ya Shirika la Umeme (Tanesco), kwa madai ya kutumwa na Mungu. Waliotiwa hatiani kwa kosa hilo, katika kesi hiyo ya jinai namba 11416 ya mwaka 2025 ni Emma…