INEC YAGAWA MAJIMBO YAANZISHA CHAMAZI NA KIVULE DAR

…………………… TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imeanzisha majimbo mapya nane nchini kote, ambapo jijini Dar es Salaam, majimbo mawili ya Chamazi na Kivule yameanzishwa kutokana na mgawanyo wa majimbo ya Mbagala wilayani Temeke na Ukonga Wilaya ya Ilala. Majimbo mapya yatakuwa sehemu ya Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka…

Read More

Wauguzi wapaza sauti wingi wa majukumu, WHO wakitoa ripoti

Dar es Salaam. Wakati dunia ikiadhimisha siku ya wauguzi, Chama cha Wauguzi Tanzania (Tanna) kimepaza sauti kuhusu upungufu wa watumishi wa kada hiyo nchini kufikia asilimia 52 kutoka 47 iliyokuwapo miaka miwili iliyopita. Wakati Tanna ikilalama kuhusu upungufu huo, Shirika la Afya Duniani (WHO), limetoa ripoti mpya inayoonyesha nchi masikini zinazalisha wahitimu wengi wa kada…

Read More

SERIKALI INABORESHA MIUNDOMBINU YA UMEME KIBITI KUONDOA CHANGAMOTO YA UMEME- KAPINGA

………………….. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inatekeleza miradi mbalimbali ya matengenezo na ukarabati wa njia za kusafirisha na kusambaza umeme katika Wilaya ya Kibiti ili kuondokana na tatizo la kukatika kwa umeme kunakotokana na uchakavu wa miundombinu hiyo. Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 12,…

Read More

Kipa Mtibwa awapiga mkwara Camara, Diarra

SAA chache baada ya kuiwezesha Mtibwa Sugar kupanda daraja na kunyakua ubingwa wa Ligi ya Championship, kipa Costantine Malimi amesema kwa sasa ameiva na yuko tayari kwa mikikimikiki ya Ligi Kuu Bara na kuonyesha ushindani dhidi ya Moussa Camara wa Simba na Djigui Diarra wa Yanga. Malimi amekuwa mhimili mkubwa kwenye mafanikio ya Mtibwa Sugar…

Read More

Kesi ya rasilimali Chadema ni pingamizi juu ya pingamizi

Dar es Salaam. Kesi ya mgogoro wa mgawanyo wa rasilimali inayokikabili Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) imegubikwa na pingamizi, kila upande ukiuwekea mwingine. Kesi hiyo, inayosikilizwa na Jaji Hamidu Mwanga katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam, imetajwa mara ya pili leo Jumatatu, Mei 12, 2025. Jopo la mawakili wa Chadema linaloongozwa na…

Read More

Kipigo cha 2-1 chaiamsha KMC FC

KICHAPO cha mabao 2-1 kutoka kwa Simba kimeizindua KMC, ambapo kaimu kocha wa timu hiyo, Adam Mbwana amesema wanayafanyia kazi makosa yaliyowaangusha juzi kwani bado kikosi kina ubora wa kuweza kuhimili vishindo wakati Ligi Kuu ikienda ukingoni. KMC ilikumbana na kipigo hicho juzi kwenye Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam ikiwa chini ya Mbwana…

Read More

Msuya aagwa, viongozi wa dini waonya rafu za uchaguzi

Mwanga. Wakati mwili wa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya, ukiagwa katika viwanja vya CD Msuya, Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro, viongozi wa dini wameonya rafu katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. Wamesema viongozi wazuri ni wale wanaochaguliwa na wananchi, na si wale wanaogawa fedha chafu kipindi cha…

Read More