Wabunge walia na utajiri kwa wageni, umasikini kwa wazawa

Dodoma. Wakati pato halisi la Taifa lilifikia Sh156.6 trilioni mwaka 2024 kutoka Sh148.5 trilioni mwaka uliotangulia, wabunge wameonyesha hofu juu ya hali ya kukua kwa uchumi wa Tanzania huku ukuaji huo ukiwa hauakisi moja kwa moja pato la Mtanzania mmoja. Katika mdahalo wa uchambuzi wa bajeti kwa wabunge uliowakutanisha wabunge na wataalam wa mipango leo…

Read More

Bajeti ilivyotumika kupoza mjadala wa usalama nchini

Dar es Salaam. Mjadala unaoendelea kuhusu matishio ya kiusalama yakiwemo matukio ya ama watu kutekwa au kuuawa ambayo yamezua wasiwasi nchini, umemlazimu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba kutumia hotuba ya Bajeti bungeni kuzungumzia hali hiyo kwa kina, akitoa hakikisho la vyombo vya dola kutuliza hali hiyo. Akiangazia hali ya ulinzi na usalama nchini, Dk Mwigulu…

Read More

TAMASHA LA ZIFF KURINDIMA JUNI 25-29 ZANZIBAR

* Filamu 430 zapokelewa kutoka Nchi za Afrika, Ulaya…… Na Leandra Gabriel, Michuzi TV MAANDALIZI ya Tamasha la Kimataifa la Filamu la Zanzibar (ZIFF,) maarufu kama Tamasha la Nchi za Majahazi msimu wa 28 kwa mwaka 2025 yamekamilika na kuelezwa kuwa litafanyika Juni 25 hadi 29 mwaka huu Ngome Kongwe Zanzibar. Akizungumza na waandishi wa…

Read More

Waliopata mafunzo ya ulinzi wa amani wafunguka

Dar es Salaam. Raia wa Watanzania waliopata mafunzo ya ulinzi wa amani yaliyotolewa na Chuo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani Tanzania (TPTC) kwa muda wa wiki moja wamesema mafunzo hayo yamewajenga darasani na kivitendo katika mchakato mzima wa ulinzi wa amani. Lengo la mafunzo hayo ilikuwa ni kuwaandaa na kuwawezesha raia kutekeleza majukumu yao…

Read More

Wataalamu, wananchi waonesha uimara, matobo ya bajeti Zanzibar

Unguja. Siku moja baada ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuwasilisha bajeti kuu kwa mwaka wa fedha 2025/2026, wataalamu na wananchi wametoa maoni tofauti kuhusu mpango huo wa kifedha. Baadhi wameipongeza bajeti hiyo wakieleza kuwa imegusa sekta mbalimbali muhimu kama elimu, afya, miundombinu na kilimo, jambo linaloashiria dhamira ya Serikali kuimarisha ustawi wa wananchi…

Read More

WAZIRI MKUU AZINDUA ALBINO MOBILE APP

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amezindua ‘Albino Mobile App’ ambayo ni program ya simu janja itakayowezasha usajili na ukusanyaji wa taarifa za watu wenye Ualbino na wenye Ulemavu kwa njia ya kidigitali. Aidha, amesema Mfumo wa Albino Mobile App ni sehemu ya Mfumo wa Kitaifa wa Taarifa za Watu…

Read More

Ndugu wawili wafariki wakitoka kwenye sherehe ya bibi

Ahmedabad, India. Dada wawili waliokuwa wakisafiri kwenda kumtembelea bibi yao kwa ajili ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa ni miongoni mwa watu waliopoteza maisha katika ajali ya ndege ya Air India. Dhir na Heer Baxi, wote wakiwa katika umri wa miaka ishirini na kitu, walitoka majumbani kwao London, Uingereza, na kuelekea Ahmedabad kwa ziara ya…

Read More

Mahakama yaidhinisha majeshi ya Trump California

San Francisco. Mahakama ya Rufaa ya Marekani imempa Rais Donald Trump ruhusa ya muda ya kuendelea kuwaweka wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi la Taifa (National Guard) katika jiji la Los Angeles. Uamuzi huo unazuia kwa sasa utekelezaji wa agizo la awali la jaji wa Serikali, ambaye alitaka kikosi hicho kirejeshwe chini ya usimamizi wa Gavana…

Read More