Polisi Mbeya yatangaza msako wamiliki magari ya shule wanaokwepa ukaguzi

Mbeya. Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya, limetangaza oparesheni maalumu ya kubaini wamiliki wa shule ambao wanakwepa kupeleka mabasi yanayosafirisha wanafunzi kukaguliwa.

Hatua hiyo imetokana na mwamko mdogo wa baadhi ya  shule kukiuka sheria sambamba na kutumia daladala za umma kusafirisha wanafunzi bila kibali.

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Alhamisi Julai 10, 2025  Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya (RTO), Mrakibu Mwandamizi wa Polisi,  SSP Notker  Kilewa, baada ya kuhojiwa kuhusiana na changamoto za ubovu wa mabasi yanayotumika kusafirisha wanafunzi  hususani kukodi  daladala za abiria, amesema kuwa kumekuwepo na kasumba ya baadhi ya wamiliki au wakuu wa shule kukwepa zoezi la ukaguzi wa mabasi ya wanafunzi na kudiliki  kutumia mabasi ya umma yasiyo na kibali.

“Tutafanya msako mkali na kwenye  Shule zote mkoani hapa  kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Ardhini (Latra ) ili kubaini wanao kwepa kutekeleza takwa  la kisheria la kufanyiwa ukaguzi  kila muhula shule zikifunguliwa,” amesema.

Amesema katika msako huo shule ambazo zitabainika mabasi ya wanafunzi kutumika bila ukaguzi hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi sambamba na kutozwa faini.

Kuhusu mabasi ya abiria kutumika kusafirisha wanafunzi, Kilewa amesema awali zipo baadhi ya shule ambazo hazina magari ya kutosha waliomba vibali ambavyo mwisho  wa kutumika ni Julai mwaka huu.

Katika hatua nyingine amewataka madereza kuwafichua wamiliki wa vyombo  vya moto wanaoshindwa kufanyia matengenezo kwa maslai yao binafsi.

Katika hatua nyingine amesema wameweza kufanikiwa kwenye  matumizi ya Mfumo wa Vithibiti Mwendo wa Mabasi (VTS) ,ambapo kwa kwa siku mabasi 30 ukamatwa yakiuka sheria za barabarani.

“Nionye madereva kutii sheria bila shuruti lakini pia toeni taariza za wamiliki wanawapa vyombo vya moto vibovu kuingiza barabara ili tuweze kufanyia kazi na kuhepuka ajali zisizo za lazima,” amesema.

Kauli za wananchi, wazazi

Ester Damian Mkazi wa Uyole jijini hapa,  amesema kumekuwa na kasumba kwa baadhi ya shule kutumia mabasi ya abiria kusafirisha  wanafunzi na kuchukua idadi  kubwa jambo ambalo ni hatari.

“Tabia hiyo imeota mizizi unakuta watoto watano wamekaa kwenye kiti ambacho wanatakiwa kukaa watu watatu, lakini wao  waangalia pesa badala ya uhai wa watoto wanaosafirishwa,”amesema

Macha amesema jambo lingine ni matumizi ya mabasi yasiyokuwa na rangi na mkanda unatambulisha ni basi la  wanafunzi na kuomba Jeshi la Polisi kulifanyia kazi.

Mmoja wa Walimu ambaye hakutaka jina lake kutajwe, amekiri kuwepo kwa changamoto ya usalama mdogo wa mabasi yanayo safirisha wanafunzi.

Related Posts