TIMU YA MKUMBI II YAWASIKILIZA WADAU MWANZA KWA MAONI YA MABORESHO YA UWEKEZAJI

Timu ya Kitaifa ya Wataalam ya kuandaa Mpango wa Pili wa Maboresho ya Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (MKUMBI II) ipo mkoani Mwanza kupata maoni ya wadau kuhusu changamoto zinazokwamisha biashara na uwekezaji nchini.

Lengo ni kupata taarifa zitakazosaidia kuandaa MKUMBI II. Utekelezaji wa MKUMBI II unatarajiwa kuongeza kasi katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ikiwa ni pamoja na kuleta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali ambazo zitaibuliwa na sekta binafsi.

Aidha, unatarajiwa utachochea uwekezaji wa sekta binafsi kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya 2050 unalenga kuwa na uchumi wa thamani ya Dola Trilioni 1 ifikapo 2050. Huku sekta binafsi ikitarajiwa kuchangia kwa asilimia 65 na kutoa ajira kwa asilimia 85.






Related Posts