SERIKALI YAZINDUA NYARAKA ZA USIMAMIZI WA MAAFA WILAYA SUMBAWANGA

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na UNDP, imezindua nyaraka tatu muhimu za usimamizi wa maafa katika Wilaya ya Sumbawanga, mkoani Rukwa.
✅ Nyaraka zilizozinduliwa:
Mpango wa Kujiandaa na kukabiliana na maafa ya Wilaya (D-EPRP)
Mkakati wa Kupunguza Vihatarishi vya Maafa (D-DRRS)
Ripoti ya Tathmini ya Vihatarishi, Uwezekano wa Kutokea na Uwezo wa kukbailian na maafa (RVCA)
📅 Uzinduzi umefanyika tarehe 23 Julai 2025 na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wananchi.
🎙️ Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Mhe. Nyakia Chirukile:
“Hii ni hatua muhimu kujenga mfumo wa utayari dhidi ya majanga kama mafuriko.”
🎙️ Brigedia Jenerali (Mstaafu) Hosea Ndagalla, Mkurugenzi wa Idara ya Maafa OWM:
“Ni utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya 2022.”
🎙️ UNDP Tanzania kupitia Bw. Godfrey Mulisa:
“Mpango huu ni sehemu ya kusaidia jamii kujenga upya maisha yao na kuwa imara zaidi.”
Wadau wa maendeleo wametoa pongezi na kuahidi kushiriki kikamilifu kutekeleza mpango huu.
🟢 #Maafa2025 #Sumbawanga #UtayariDhidiYaMajanga #UNDP #OWM