WAZIRI GWAJIMA KUZINDUA KAMPENI YA ‘BADILIKA’ TOKOMEZA UKATILI MKOANI KIGOMA

 

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum- Dkt. Doroth Gwajima anatarajiwa kuzindua kampeni ya ‘Badilika, Tokomeza Ukatili’ yenye lengo la ukatili wa kijinsia mkoani Kigoma.

Uzinduzi huo umepangwa kufanyika Jumatatu Julai 28, 2025 katika uwanja wa Mwanga Community Centre ambapo kampeni hiyo inatarajiwa kuleta hamasa makundi ya kijamii kuwa wanamabadiliko kupitia elimu itakayotolewa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la kutetea haki za watoto na wanawake la KIVULINI, Yassin Ally amesema kampeni hiyo inawezeshwa na shirika la maendeleo la Ubelgiji (ENABEL), linalosaidia utekelezaji wa miradi ya kutokomeza ukatili wa kijinsia mkoani Kigoma.

Elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kijamii na kiuchumi inatarajiwa kutolewa kwenye uzinduzi huo huku burudani ikinogeshwa na msanii wa nyimbo za Singeli, Dogo Paten.

Tazama Video hapa chini