
Wafanyakazi wa Kampuni ya Barrick nchini wakifurahia baada ya kumaliza mbio za NBC Dodoma Marathon
***
Kampuni ya Barrick nchini imekuwa na program za mazoezi kwa ajili ya kuhakikisha wafanyakazi wake wanakuwa na nguvu na afya bora.
Kila mwaka kampuni imekuwa ikiwezesha wafanyakazi wake kushiriki riadha mbalimbali na michezo ndani na nje ya nchi ikiwemo mbio za kilomita 42 za Bulyanhulu Healthy Lifestyle Marathon zinayofanyika kila mwaka.
Migodi yake ya North Mara na Bulyanhulu pia imewekeza kujenga miundombinu ya michezo na mazoezi ili kuwawezesha wafanyakazi wake kushiriki michezo na mazoezi katika mazingira rafiki kwa ajili ya kujenga afya zao.
Lengo kuu la mbio hizi zilizowashirikisha maelfu ya wakimbiaji kwa mujibu wa waandaaji Benki ya NBC lilikuwa ni kukusanya fedha ili kusaidia mapambano dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi , kutoa ufadhili wa elimu kwa wakunga ili kusaidia watoto wenye changamoto ya ugonjwa wa usonji na kampeni dhidi ya Saratani ya kizazi na jumla ya shilingi milioni 700 zilipatikana.
Picha mbalimbali za wafanyakazi wakifurahia baada ya kumaliza mbio za NBC Dodoma Marathon