KIKWETE NA MALALA WAONYA: BAJETI ZA ELIMU ZISIPUUZWE WAKATI WA MISUKOSUKO YA KIUCHUMI NA KISIASA DUNIANI

Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Malala Yousafzai, wameonya juu ya mwenendo hatarishi duniani wa kupunguza au kupuuza bajeti za elimu hasa wakati wa misukosuko ya kiuchumi na kisiasa. Wakizungumza kwenye mjdala kuhusu elimu uliofanyika Jumapoili usiku katika hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam, viongozi hao…

Read More

Serikali yatangaza ajira mpya, omba hapa

Dar es Salaam. Serikali imetangaza nafasi mpya 526 za kazi kwa Watanzania wenye sifa zinazohitajika, katika taasisi mbalimbali za umma zikiwamo hospitali ya Muhimbili (MNH), Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (Tawa), Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Chuo cha Mweka na nyinginezo. Tangazo hilo lililotolewa jana Julai 14, 2025, linaainisha kuwa nafasi hizo ni kwa…

Read More

Mabishano ya tozo yakwamisha Tanga kufikia malengo

Dodoma. Mabishano ya tozo katika bidhaa zinazozalishwa na madini, yamesababisha Mkoa wa Tanga kushindwa kufikia lengo walilopangiwa katika makusanyo kwa mwaka 2024/25. Aidha, wastani wa pato la mtu mmoja mmoja kwa mwaka limeongezeka kutoka Sh2.7 milioni mwaka 2020 hadi Sh3.4 milioni kwa mwaka 2024. Akizungumzia mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita, kwa mkoa wa…

Read More

Tanzania, Kenya na Uganda zaombwa kunusuru vyanzo vya maji, kilimo cha umwagiliaji kikipigiwa chapuo

Mbeya. Ili kunusuru vyanzo vya maji na kuongeza hali ya uzalishaji wa chakula, wataalamu wameshauri nchi za Afrika Mashariki kushirikiana kimkakati kuzuia shughuli za kijamii katika maeneo hayo. Pia, wameshauri namna ya kuepukana na mabadiliko ya tabianchi na kukuza kilimo chenye tija ni kuweka mazingira mazuri kwa wakulima na kuwapa mbinu za matumizi sahihi ya…

Read More

Mrisho Mpoto Afiwa Na Mkewe – Global Publishers

Mrisho Mpoto, msanii wa sanaa za maonesho na kughani Mrisho Mpoto, msanii wa sanaa za maonesho na kughani, kupitia akaunti yake ya Instagram ametoa taarifa za kufiwa na mkewe ambaye alikuwa akiugua. Akizungumza na mwandishi wa Global TV, Mpoto amethibitisha taarifa hizo na kueleza kuwa alikuwa akisumbuliwa na presha kwa muda mrefu….

Read More

Mvuvi afa baharini akivua dagaa, mwingine atoweka

Kilwa. Mvuvi Mussa Kibarabara (25), mkazi wa Wilaya ya Kilwa, amefariki dunia wakati akivua dagaa katika Bahari ya Hindi, huku mwingine akiripotiwa kupotea. Akizungumza na Mwananchi leo Jumanne, Julai 15, 2025 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi John Imori amesema kuwa Kibarabara alikwenda kuvua dagaa Jumatatu ya Julai 13, 2025 majira ya usiku katika pwani…

Read More

Vigogo Chadema waachiwa kwa dhamana, kuripoti tena kesho

Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimethibitisha kuwa viongozi wake wawili wakuu, Brenda Rupia ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi pamoja na Leonard Magere, Mkurugenzi wa Rasilimali, Miradi na Uwekezaji, wameachiwa kwa dhamana baada ya kushikiliwa na Jeshi la Polisi. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na chama hicho leo Jumanne, Julai…

Read More