DC MPOGOLO ATUNIKIWA TUZO – MICHUZI BLOG

 MTANDAO  wa Polisi Wanawake Tanzania  (TPF-Net) Wilaya ya Ilala umemtunuku tuzo maalumu Mkuu wa  wilaya hiyo Edward Mopogolo ya  kutambua mchango wake katika  kujenga jamii salama,jumuishi na yenye usawa wa kijinsia 

DC Mpogolo amekabidhiwa tuzo hiyo  ofisini kwake jijini Dar es Salaam, leo.

Aliushukuru mtandao TPF Net  kwa kutambua mchango huo na kwamba tuzo hiyo ni heshima kubwa kwake na wananchi wa Wilaya ya Ilala.

Tuzo hiyo ilikabidhiwa na SSP Latifah Chicco (RFBO Ilala),ASP Sophia Dilunga (OCS Kati na A/Inspekta  Husna wa Ofisi ya  RFBO Ilala.