Dodoma. Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, mkoani Dodoma, Simon Mayeka amewashangaa baadhi ya vijana waliojitokeza kushangilia baada ya kutangazwa kwa taarifa za msiba wa aliyekuwa Spika wa Bunge, Job Ndugai.
Akizungumza leo Alhamisi Agosti 7, 2025, baada ya kufika nyumbani kwa Ndugai ulipo msiba, Mayeka amesema ni kitu kinachoshangaza kwa sababu hiyo siyo mila wala desturi za Kitanzania.
Hivyo, amewaomba wananchi wa Kongwa kuwa watulivu wakati huu wa msiba na kuwaomba wazazi wakemee vijana kwa kuwa hakuna uadui wa kushangilia mauti.
Endelea kufuatilia Mwananchi.