Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniface Mwabukusi, leo tarehe 27 Agosti 2025, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma.
Mazungumzo hayo yalihusu masuala mbalimbali yanayohusiana na sekta ya sheria nchini, ikiwemo nafasi ya wanasheria katika kukuza demokrasia, utawala wa sheria, na haki za wananchi.
Ikulu imesema kikao hicho ni sehemu ya jitihada za Serikali kuendelea kushirikiana na wadau wa kisheria kwa ajili ya kuimarisha misingi ya haki na uwajibikaji nchini.
Related