Rais Mwinyi afafanua ongezeko la usawa wa kijinsia Zanzibar
Unguja. Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi amesema Zanzibar imepiga hatua katika masuala ya usawa wa kijinsia kuanzia kwenye sera na sheria zilizopo. Amesema Serikali imeanza utekelezaji wake kuhakikisha usalama wa wanawake unazingatiwa kwa kuweka miundombinu bora kwao. Dk Mwinyi ameeleza hayo leo Jumanne Agosti 26, 2025 katika ufunguzi wa mkutano wa saba wa dunia…