18 wapenya usaili RT,  Ikangaa, Isangi wajiondoa

Kuelekea uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), unaotarajiwa kufanyika Agosti 16 mwaka huu jijini Mwanza, wagombea 18 wamefaulu katika mchujo wa awali. Mchakato huo umetawaliwa na matukio ya kushtua ikiwemo kujiondoa kwa nyota wa zamani wa riadha nchini, Juma Ikangaa  pamoja na rais aliyemaliza muda wake, Silas Isangi ambao walitangaza uamuzi huo wakiwa…

Read More

Kwa Mkapa kila kitu shwari

UTARATIBU wa kuingia Uwanja wa Benjamin Mkapa unaotarajiwa kupigwa mechi ya ufunguzi wa michuano ya Chan kati ya Tanzania na Burki Faso umezingatia ustaarabu. Kabla ya mageti kufunguliwa nyomi ya watu ilijaa nje ya uwanja, wakisubiri kuingia ili kushuhudia mechi hiyo inayotarajiwa kuchezwa kuanzia saa 2:00 usiku, lakini baada ya kuruhusiwa kila kitu kinakwenda bila…

Read More

CHAN yabadili utaratibu kwa Mkapa

TOFAUTI na ilivyozoeleka katika mechi nyingi za ndani, ambapo mageti ya viwanja hufunguliwa mapema ili kuwapa mashabiki nafasi ya kuingia mapema, hali imekuwa tofauti kwenye ufunguzi wa mashindano ya CHAN 2024. Uwanja wa Benjamin Mkapa ambao utatumika kwa ufunguzi wa mashindano hayo ulinzi ni mkubwa  huku mashabiki wakizuiwa kuingia mapema kama ilivyo kawaida. Mashindano hayo…

Read More

Jezi Stars ndio habari kubwa

Hapa Uwanja wa Benjamin Mkapa, uzalendo umewekwa mbele kwa mashabiki wengi kuvaa jezi za timu ya taifa badala ya zile za klabu. Tanzania kupitia Taifa Stars, leo itacheza mchezo wa ufunguzi wa Fainali za Mataifa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), itakapokutana na Burkina Faso, mechi itakayoanza saa 2:00 usiku. Nje ya uwanja wa Mkapa…

Read More

Vilio vya wafanyabiashara Kwa Mkapa

LICHA ya mashabiki waliojitokeza kwa wingi nje ya Uwanja wa Mkapa hali kwa wafanyabiashara sio nzuri baada ya kulalamikia biashara kutokwenda kama matarajio yao. Nyomi iliyojitokeza hapa ikisubiri muda wa kuruhusiwa kuingia ndani wengi wamekuwa wakizunguka zunguka kuvuta muda huku wengine wakijipumzisha maeneo ya vivuli. Wakizungumza na Mwanaspoti, wafanyabiashara waliopo nje ya Uwanja wa Mkapa…

Read More

Bares ataja la kujifunza Chan

ALIYEKUWA kocha wa Tanzania Prisons, Abdallah Mohamed ‘Bares’ amesema kuna la kujifunza katika Fainali za Ubingwa kwa Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024 kimbinu, ufundi na uzalendo kupitia mechi mbalimbali zitakazochezwa. Alitoa wito kwa makocha na wachezaji kutenga muda wa kuifuatilia michuano hiyo, ili kupata kitu cha kujifunza kutoka katika mataifa mbalinbali yaliyopo nchini. “Michuano hiyo…

Read More

Taifa Stars Stars kuvuna Sh9.9 bilioni

MICHUANO ya Fainali za Ubingwa kwa Mataifa ya Afrika  kwa wachezaji wa ndani (CHAN) 2024 inaanza leo, Agosti 2, 2025 kwa mechi ya ufunguzi kati ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya Burkina Faso itakaochezwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Kuanza kwa michuano hiyo kunaifanya Stars mezani kuwa na kitita cha Sh9 bilioni…

Read More

Hali ilivyo Uwanja wa Mkapa

MIONGONI mwa kauli alizozitoa kipa wa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Aishi Manula aliyetoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi ili kuisapoti katika mechi ya ufunguzi wa Kombe la Mataifa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) dhidi ya Burkina Faso, alisema: “Tupo katika ardhi ya nyumbani, Watanzania waje ili tujisikie nguvu ya kupambana.”…

Read More