Mafuriko yaua watu watatu, yaacha zaidi ya 100 bila makazi

Kampala. Watu watatu wamefariki dunia huku zaidi ya watu 100 wakipoteza makazi baada ya mafuriko makubwa kuyakumba maeneo ya Mbale na Sironko nchini Uganda. Taarifa iliyotolewa na tovuti ya habari ya Daily Monitor ya Uganda imeeleza kuwa mafuriko hayo yamesababishwa na mvua kubwa zilizoanza kunyesha tangu Jumapili, Agosti 17, 2025, na kusababisha uharibifu wa miundombinu…

Read More

Jaji Mkuu akemea watuhumiwa kunyimwa dhamana

Dodoma. Jaji Mkuu wa Tanzania, George Masaju amekemea tabia ya baadhi ya mahakimu kuwanyima dhamana watuhumiwa ambao kesi zao zinadhaminika akisema kitendo hicho ni kiashiria cha kutaka rushwa. Jaji Masaju amesema kesi yoyote ambayo inaangukia katika kifungu cha dhamana, ni muhimu watuhumiwa wakapewa siku hiyohiyo ili kukwepa msongamano magerezani na ataanza kulifuatilia jambo hilo mwenyewe….

Read More

Suti ya kijeshi ya Zelenskyy yazua mjadala

Dar es Salaam. Baada ya kusakamwa kutovaa suti kwenye mkutano wa Rais Donald Trump uliopita, Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy hatimaye katika mkutano wa jana wa kutafuta amani ya Ukraine na Russia, alionekana amevaa suti ya kijeshi hatua iliyoibua mada mpya. Katika mkutano uliopita mapema mwaka huu kati ya Trump na Zelenskyy na Makamu wa…

Read More

Mabaharia wa Kitanzania wajipanga kuzikabili changamoto

Dar es Salaam. Chama cha Watanzania waliohitimu katika Chuo Kikuu cha Bahari Duniani (WMU) kinakusudia kuwaleta pamoja wataalamu katika sekta hiyo ili kushirikiana kitaaluma na kusaidiana katika kushughulikia changamoto na fursa katika sekta ya bahari kitaifa na kikanda. Chama hicho kinachojulikana kama Chama cha Wahitimu wa WMU Tanzania (WMUTAA), kilisajiliwa rasmi Aprili 2025 baada ya…

Read More

Waliofariki kwa kufukiwa na kifusi mgodini wafikia watano

Shinyanga. Mwili wa mtu mmoja umeopolewa katika mgodi wa Chapakazi na kufikisha idadi ya waliofariki dunia baada ya kufukiwa na kifusi kwenye mgodi huo kufikia watu watano, huku watatu wakitolewa wakiwa hai. Agosti 11, 2025, wafanyakazi na mafundi zaidi ya 22 wa mgodi huo walifukiwa kwenye mashimo baada ya kutitia wakati wakifanya ukarabati wa mduara…

Read More