::::::::
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Chama Cha Mapinduzi kimesema kwa mujibu wa Sheria hakuna chama chochote cha Siasa ,Vyombo vya habari au Taasisi yoyote yenye Mamlaka ya kutangaza matokeo ya Uchaguzi bila idhini ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).
Pia chama hicho kimesisitiza kuwa Uchaguzi katika nchi yoyote duniani , huongozwa kwa kanuni na taratibu za kisheria si kwa mtindo holela .
Msimamo huo umetolewa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Idara ya Itikadi ,Uenezi na Mafunzo, Khamisi Mmbeto Khamis, wakati akijibu hoja zilizotolewa na mgombea urais wa ACT Wazalendo ,Othman Masoud Othman .
Othman mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania Urais, amesikika akiikosoa Sheria ya Kura ya mapema akitishia na kutaka iisitumilke .
Mbeto akijibu hoja hiyo alisema ,sheria hiyo haikiutungwa aidha na Malaika ,majini au Mashetani , bali imetungwa na binadamu waliopewa dhamana ya kutunga na kupitisha sheria.
Alisema sheria hiyo itaendelea kutumika Zanzibar hadi pale Baraza la
Wawakilishi Zanzibar, litakapofanya mabadiliko mengine kwa utaratibu halali .
“Hakuna Sheria nzuri au mbaya ikiwa imeshatungwa pia imepitishwa na Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Sheria ya Kura ya mapema imeridhiwa na chombo hicho .Haikutungwa katika ofisi ya chama chochote cha Siasa” Alisema Mbeto
Aidha, Katibu huyo Mwenezi alisema ni wazi ACT kupitia mgombea wake wa urais , kimebaini kushindwa kwa kuona maendeleo yalivyoshamiri huku wananchi wakisifu uongoozi wa Rais Dk Hussein Ali Mwinyi .
“Hayupo mwenye ubavu wa kuzuia watu wasipige kura ikiwa sheria inataka hivyo . Atakaewatisha, kuwazuia au kutaka kuwapiga Wapiga Kura wasifike vituoni watadhibitiwa na mkono wa sheria “Alisema Mbeto
Pia katibu huyo Mwenezi aliongeza kusema kuwa ikiwa Othman ameshajua kuwa hawezi kushinda ,si kosa kwake kutangaza kuwa amekubali kushindwa .
“Sheria anayoipinga imetungwa na Wajumbe halali wa Baraza la wawakilishi Zanzibar . Inawezaje kufutwa leo ikiwa chombo hicho kimevunjwa kisheria ?” Alihoji Mbeto
Mwenezi huyo alisema anachokitaka Othman ni kuwashawishi Vijana wa ACT ili walete ghasia na fujo kwa kisingizio cha Sheria ya kura za mapema ambayo imekuwa ikitumika katika Mataifa mengi duniani.