TUME YAKAGUA MAANDALIZI YA UCHAGUZI MKUU MAFINGA MJI, WASISITIZWA WELEDI

 Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Septemba 21, 2025 ametembelea  Halmashauri ya Mji wa Mafinga Wilayani Mufindi Mkoani Iringa ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ambapo pamoja na mambo mengine alipokea taarifa ya Mji huo kutoka kwa wasimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri kuhusu maandalizi ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2025 na kisha kukagua vifaa ambavyo tayari vimepokelewa katika Halmashauri hiyo.  

Jaji Mwambegele yupo Mkoani Iringa kukagua maandalizi hayo na kutazama kampeni za wagombea katika majimbo ya Mkoa wa Iringa 

kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa na Tume,Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 unatarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu. 

“Kura Yako Haki Yako Jitokeze Kupiga Kura”

Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa Bi. Nuru Sovella akizungumza jambo wakati wa utoaji wa taarifa maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele

Msimamizi Jimbo la Mafinga Mjini Mwalimu Doroth Kobelo akiwasilisha taarifa ya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele (katikati) kulia ni Mratibu wa Uchaguzi Mkoa wa Iringa, Bi. Nuru Sovella.