WIZARA YA UJENZI, TANROADS, POLISI WAKAGUA MAENEO YENYE AJALI ZA MARA KWA MARA KATIKA MTANDAO WA BARABARA NCHINI

::::::::

Wizara ya Ujenzi kupitia Kitengo cha Usalama na Mazingira kinaendelea na utekelezaji wa ukaguzi wa maeneo hatarishi katika mtandao wa Barabara kuu nchini. Aidha kwa sasa ukaguzi huo unafanyika katika shoroba ya TANZAM inayoanzia katika Mkoa wa Dar es Salaam hadi Mkoani Songwe kupitia Morogoro (Mikumi) na baadaye katika shoroba zingine

Ukaguzi huo unahusisha wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi, Wakala wa Barabara (TANROADS) , Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Usalama Barabarani pamoja na wadau wengine ambapo watakagua maeneo yote yenye changamoto za ajali za mara kwa mara na kupendekeza hatua za muda mfupi, wa kati na mrefu ili kutatua changamoto hizo na kupunguza vifo na majeruhi vitokanavyo na ajali.