Mbeya. Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025, Ismail All Ussi ameagiza kuwepo mkakati wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi mashuleni ili kutunza mazingira na kuunga mkono agizo la Rais Samia Suluhu Hassan.
Ussi amesema hayo leo Alhamisi Oktoba 9, 2025 wakati akiweka jiwe la msingi kwenye bwalo la wanafunzi wa Shule ya Sekondari Imezu Wilaya ya Mbeya sambamba na kugawa mitingi ya nishati safi bure kwa kaya maskini wakazi wa vijiji vya Inyala na Itewe.
Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka 2025,Ismail Ussi(kuli ) akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi wa bwalo la Shule ya Sekondari Imezu Wilaya ya Mbeya.Picha na Hawa Mathias
“Nendeni mkaunge mkono kampeni za Rais Samia Suluhu Hassan juu ya matumizi ya nishati safi ili kutunza mazingira haswa matumizi ya gesi ambayo ni salama kwa afya za watanzania,”amesema.
Amesema ni jukumu la kila mwananchi kugeukia matumizi ya nishati safi ya gesi ili ifikapo 2030 tufikie asilimia 80 lakini tuna kila sababu kuipongeza Serikali ya Wilaya kuendelea kusimamia wajibu kwa kutoa mitungi ya gesi kwa wananchi kaya maskini, “amesema.
Ussi amesema ufike wakati walimu mashuleni kubebe jukuhu hilo kama ajenda ya kutoa elimu kwa wanafunzi ili kutimiza matakwa ya Serikali ili kutunza mazingira.
Katika hatua nyinyine, amewataka wananchi hususani wanafunzi kuhamasisha wazazi kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu Oktoba 29,2025 kupiga za mgombea urais Samia Suluhu Hassan.

Muonekano wa bwalo la wanafunzi wa Shule ya Sekondari Imezu Wilaya ya Mbeya lililowekwa jiwe la msingi na mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2025.Picha na Hawa Mathias
“Lakini pia nimeona Serikali ya Mkoa wa Mbeya imesimamia vyema utekelezaji wa miradi ya maendeleo sambamba na uwezeshaji makundi ya wanawake, vijana na walemavu na ndio lengo la Serikali ya awamu ya sita,”amesema.
Ussi pia amepongeza uongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa usimamizi mzuri wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Sh1.3 bilioni ambayo imekaguliwa na mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa 2025.
“Niwasihi endeleeni kusimamia vyema utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo Serikali ya awamu ya sita imetoa fedha kwa maslai ya Watanzania na Taifa kwa ujumla,”amesema.

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Solomon Itunda, akitoa taarifa ya mradi wa ujenzi wa bwalo la Shule ya Sekondari Imezu Wilaya ya Mbeya kwa kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ussi. Picha na Hawa Mathias
Wakati huo huo ameonyesha kuridhishwa na utekelezaji wa mradi wa kuzalisha hewa tiba (Oxygen Plant), wenye thamani ya Sh298 milioni ambao utaleta tija katika hospitali vituo vya afya na zahanati.
Mradi huo una uwezo wa kuzalisha mitingi hewa tiba 90 yenye ujazo wa lita kwa masaa 24 na kutoshereza mahitaji ya hosptali kwa mahitaji ya mitungu 10 hadi 15 kwa siku jambo ambalo litaboresha utoaji wa huduma za afya.
Awali Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Solomon Itunda ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa miradi mingi ya maendeleo.
“Tunaishukuru sana Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, lakini tutahakikisha anapata kura za kishindo katika uchaguzi mkuu Oktoba29,2025, “amesema.

Mjasiriamali wa kuchoma nyama katika kituo cha mabasi Tarafani, Sambe Joel amesema wameweza kufanikiwa kiuchumi kufuatia mikopo asilimia 10 iliyotolewa na Serikali.
“Tuko bega kwa bega na Mama Samia tumeona alivyoweza kupunguza uharifu nitaani kwa kutoa mikopo,lakini tunaomba aelekeze halmashauri kuondoa ukiritimba wa utoaji wa mikopo jambo ambalo linawakatisha tamaa na kuitwisha mzigo Serikali, “amesema.