Na Yohana Kidaga- Kipugira
Mgombea wa Ubunge jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa amesema endapo wananchi watampa ridhaa ya kumchagua tena katika kipindi hiki atakwenda kusimamia maendeleo ya wananchi wa Jimbo hili, huku akimwombea kura Mhe Rais Samia.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi katika kata ya Kipugira Mhe. Mchengerwa amesema katika kata hilo endapo atachaguliwa atakwenda kuishawishi Serikali kukamilisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mloka hadi Mkongo ili ipitike katika kipindi chote cha mwaka.
Katika hatua nyingine, Mhe. Mchengerwa amefafanua kuwa siasa zake ni za maendeleo ya kwa maana ya kwamba siasa zake zimelenga katika kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli na siyo ujanja ujanja.
Mhe. Mchengerwa metumia mkutano huo kutaja mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi chote cha miaka kumi cha mabadiliko ya fikra kwa wananchi wa Rufiji.
Leo Mhe Mchengerwa anaendelea na mikutano ya hadhara katika kata nyingine za Jimbo hilo kuomba kura kwa Rais Samia Suluhu Hassan, kwa madiwani na kwake mwenyewe ili apewe ridhaa ya kuwaongoza tena katika kipindi hiki.
Mhe Mohamed Mchengerwa ni Mbunge wa tisa wa kuchaguliwa katika jimbo hilo la Rufiji toka lianzishwe na kuongozwa na wabunge kadhaa kuanzia Mhe. Bibi Titi Mohamed ambapo anaelezewa kuwa ni miongoni mwa wabunge walioliletea maendeleo makubwa Jimbo hilo ukilinganisha na wabunge waliotangulia.