Kuleta mapinduzi katika biashara na urahisi wa malipo kwa wateja na wafanyabiashara wa Tanzania.
Kupitia ushirikiano na VISA, Alipay, Network International, Magnati na MTN Uganda, wateja sasa wanaweza kufanya malipo kwa kutumia mfumo wa Tap & Pay duniani kote kwa kugusisha simu yenye M-Pesa Visa card kwenye mashine ya malipo, kulipa wafanyabiashara nchini China kupitia Alipay kwa mfumo unaowezeshwa na Thunes, kufanya miamala Dubai kwa wafanyabiashara waliounganishwa kwenye mfumo wa TerraPay, pamoja na kuwalipa wafanyabiashara nchini Uganda moja kwa moja kwenye waleti zao za MTN MoMo., yote haya kupitia M-Pesa Super App au Menyu ya M-Pesa.
Huduma hizi ni salama, rahisi kutumia na zinaondoa changamoto zinazotokana na mifumo ya kibenki. Kwa pamoja, huduma hizi zimeifanya M-Pesa kuwa moja ya mifumo ya malipo ya kidigitali iliyoendelea zaidi barani Afrika.
Epimack Mbeteni, Mkurugenzi wa M-Pesa Vodacom Tanzania, alisema: “Ushirikiano wetu na VISA, Alipay, Network International na MTN Uganda unaonyesha dhamira yetu ya kujenga mifumo imara ya malipo ya kidigitali. Kwa pamoja, tunawawezesha watu kufanya malipo hata wavukapo mipaka ya Tanzania kwa urahisi ule ule wanaoufanya ndani ya nchi, kwa usalama, haraka na kwa gharama nafuu,” alisema Mbeteni.
Uzinduzi huu unaleta ubunifu mpya uitwao M-Pesa Tap & Pay kwa ushirikiano na Visa, ubunifu wa kwanza barani Afrika, unaowawezesha wateja kulipa duniani kote kwa kugusa tu simu zao zenye M-Pesa Visa card kwenye machine za watoa huduma zenye mfumo wa Visa. Victor Makere, Meneja wa Nchi wa Visa Tanzania, alisema: “Kupitia ushirikiano huu, tunawawezesha mamilioni ya wateja wa M-Pesa kufurahia malipo ya kidigitali yaliyo salama na rahisi popote Visa inapokubalika.
Kupitia Mtandao wa Thunes, wateja wa M-Pesa sasa wanaweza kulipa wafanyabiashara nchini China ndani wanaotumia mfumo wa Alipay kwa kasi na usalama.
TerraPay, ambayo inawezesha malipo ya kimataifa kwa wafanyabiashara, inawaruhusu watumiaji wa M-Pesa kufanya miamala na wafanyabiashara waliopo Dubai kupitia mtandao wao mpana wa malipo.
Kwa upande wa malipo kidigitali nchini Uganda kupitia MTN MoMo, MTN ina mchango muhimu katika kurahisisha biashara za kikanda kwa wajasiriamali wadogo na wa kati. Richard Yego, Mkurugenzi wa MTN Mobile Money Uganda, alisema: “Ushirikiano huu ni hatua muhimu kuelekea biashara huru na endelevu katika ukanda huu.
Kwa kuzingatia matumizi makubwa ya huduma za fedha kwa simu na ongezeko la simujanja nchini Tanzania, masuluhisho haya ni nyenzo muhimu kwa wateja wa kawaida pamoja na biashara ndogo na za kati zinazohitaji huduma za kifedha za uhakika, za haraka na rahisi.
M-Pesa ikiendelea kupanuka kama huduma salama na rahisi ya malipo ya kimataifa, Vodacom Tanzania inaendelea kutekeleza dhamira yake ya kujenga uchumi jumuishi wa kidigitali na kubadilisha maisha kupitia teknolojia.
